• Mtayarishaji wa maudhui Dem Wa Facebook amevujisha picha ya skrini ya mazungumzo aliyokuwa nayo na baba wa watoto wake siku ya Father’s Day
  • Mshawishi huyo wa mitandao ya kijamii alijifungua watoto mapacha wa kike mwezi Mei na alishiriki habari hiyo na wafuasi wake karibu mwezi mmoja baadaye
  • Wakati Dem Wa FB alipotangaza ujauzito wake, Wakenya wengi walikuwa na hamu ya kujua baba wa watoto wake ni nani

Awali alikuwa ameeleza kuwa baba wa watoto wake si mtu anayependa kuonekana hadharani, na alitaka kumlinda dhidi ya macho ya umma.

Dem Wa FB (kushoto), alivujisha gumzo (kulia).
Dem Wa Fb alivujisha gumzo na mpenzi wake. Picha: Dem Wa FB.
Source: Facebook

Mtayarishaji huyo wa maudhui alitoa mifano ya mastaa wengine wanaoshiriki hadithi zao za mapenzi mtandaoni na jinsi Wakenya wanavyochambua kila jambo katika maisha yao.

Wakati wa sherehe yake ya baby shower, Wakenya walitarajia kumuona baba huyo wa watoto, lakini aliwaalika watu wake wa karibu pekee na hakuna aliyeshiriki maelezo kuhusu siku hiyo maalum.

Wakenya walimsifu kwa kuwa na marafiki wanaoweza kutunza siri, ambao waliweka sherehe hiyo kuwa siri hadi alipotoa picha mwenyewe.

Pia soma

Nairobi: Mwanafunzi wa Gredi ya 9 afariki baada ya kuwasili shuleni alfajiri, mzazi alia kwa uchungu

Kujifungua kwake pia kulifanywa kwa usiri mkubwa, huku mastaa kadhaa wakiwa karibu naye, akiwemo mwigizaji wa Papa Shirandula, Jacky Vike maarufu kama Awinja.

Siku ya Father’s Day, Wakenya walitarajia angemsherehekea baba wa watoto wake hadharani, lakini alichovujisha ni ujumbe wa WhatsApp aliomtumia.

Katika maelezo yake, aliwahakikishia mashabiki wake kwamba hawatawahi kujua yeye ni nani.

Aliandika:

“Huyu naye huku online hamtawai muona. I definitely wished Baba Twins a happy Father’s Day.”

Dem Wa FB alikuwa amemhifadhi kwenye simu yake kwa jina la “My Love”, na aliandika ujumbe mrefu akimpongeza kama mwenzi bora na baba wa kipekee kwa mabinti wao.

“Happy Father’s Day, my love❤️ Leo ninasherehekea mwanaume wa ajabu ulivyo; si kwangu tu bali pia kwa mabinti wetu wazuri, [majina yamefichwa kwa sehemu]. Asante kwa kuwa baba mwenye bidii, anayekuwepo wakati wote, mwenye upendo na aliyejitolea kwa watoto wetu. Jinsi unavyowajali mabinti wetu kila siku huwa haipiti bila kutambuliwa.”

Mshawishi huyo wa mitandao pia alitania kuhusu kumnunulia mwenzi wake gari aina ya G-Wagon na akatangaza upendo wake kwake katika ujumbe huo wa kugusa moyo.

Pia soma

“Acheni Kumshambulia Baba Yangu”: Sky Victor Amtetea Tash Kufuatia Madai ya Pesa

“Asante kwa kunifanya mama na kwa kunipa zawadi hii ya ajabu ya umama. Asante kwa kuendelea kuniamini, kunisukuma nikue, kufuatilia ndoto zangu na kuwa toleo bora zaidi la nafsi yangu. Ninashukuru sana kushirikiana nawe safari hii ya maisha. [Majina yamefichwa kwa sehemu] na mimi tumebarikiwa sana kuwa nawe. Ninge kununulia G-Wagon, lakini nasikia huko ilipo ni bei nafuu zaidi ama ununue tu nitakurefund. Happy Father’s Day, my love. Tunakupenda bila mwisho.”

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *