
Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa, uamuzi wa kusitisha mapigano nchini Lebanon umetolewa baada ya Marekani kutoa mashinikizo makali dhidi ya Tel Aviv na kwamba, maafisa wa kisiasa wa utawala huo wamesalimu amri tena kwa masharti ya Iran.
Kwa mujibu wa Pars Today, ikinukuu Shirika la Utangazaji la Iran, Idhaa ya 12 ya TV ya Israel iliripoti, ikitoa vyanzo vya habari, kwamba uamuzi wa kusitisha mapigano nchini Lebanon ulifanywa baada ya Marekani kuweka shinikizo kwa Tel Aviv.
Kanali ya 12 ya Televisheni ya Israel cha ilisema kuwa, kuna ukimya kabisa Israel kutokana na maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na Waziri wa Ulinzi Yisrael Katz kuhusu kusitisha mapigano nchini Lebanon.
Wakati huo huo, Kanali ya 13 ya Televisheni ya Israel pia ilitangaza ikitoa mfano wa chanzo cha kidiplomasia, kwamba Washington, katika ujumbe rasmi, iliitaka Tel Aviv kujiepusha na ongezeko lolote la mvutano nchini Lebanon ili kutoa fursa ya kuendelea mazungumzo nchini Uswisi.
Chombo cha habari cha Kiebrania Walla, katika uchanganuzi wake wa hali mpya, kiliripoti kwamba jeshi la Israel limebanwa tena na mashinikizo ya Iran na kwamba “mlingano huu mpya” unatawala uwanjani.
Katika anga hiyo hiyo, Ehud Olmert, Waziri Mkuu wa zamani wa utawala wa Kizayuni amemtaka Benjamin Netanyahu aondoke madarakani.
Olmert, akikosoa vikali utendakazi wa Netanyahu, amesema kuwa Waisraeli wengi hawatamsamehe kwa kushindwa kwake na kwamba sera zake zimekuwa zikifeli tangu mwanzo.
Wakati huo huo, uchunguzi mpya wa maoni katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu unaonyesha kuwa wakazi wengi katika maeneo hayo wanataka Netanyahu aondoke kwenye ulingo wa siasa. Kulingana na kura ya maoni iliyofanywa na kituo cha televisheni cha Israel Channel 12, takriban asilimia 60 ya waliohojiwa wanaamini kuwa Netanyahu hapaswi kugombea tena nafasi ya waziri mkuu katika uchaguzi ujao.