f

Chanzo cha picha, Getty Images

Senegal imeondolewa kwenye Kombe la Dunia 2026 kwa njia ya kusikitisha baada ya kupoteza mabao 3-2 dhidi ya Ubelgiji katika muda wa nyongeza, licha ya kuwa ilikuwa inaongoza kwa mabao mawili hadi dakika za mwisho za mchezo.

Matokeo hayo yanaifanya Senegal kuwa timu ya tano kutoka Afrika kuaga mashindano hayo, ikiifuata Afrika Kusini, Ivory Coast, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Tunisia.

Kwa sasa, Morocco ndiyo timu pekee ya Afrika iliyofuzu hatua ya 16 bora baada ya kuwaondoa Uholanzi kwa mikwaju ya penalti.

Algeria, Misri, Cape Verde na Ghana bado zinasaka nafasi ya kuungana nao.

Senegal ilianza vyema mechi hiyo ya hatua ya 32 bora mjini Seattle, ikitangulia kwa bao la Habib Diarra dakika ya 25 kabla ya Ismaila Sarr kuongeza la pili dakika ya 51 na kuifanya ionekane kuwa njiani kutinga hatua inayofuata.

Hata hivyo, ndani ya dakika tatu za mwisho za muda wa kawaida, Belgium ilibadili kabisa mchezo. Romelu Lukaku, aliyeingia akitokea benchi, alifunga dakika ya 86 kabla ya nahodha Youri Tielemans kusawazisha dakika ya 89 na kuupeleka mchezo katika muda wa nyongeza.

Senegal ilijitahidi kuhimili shinikizo katika muda wa nyongeza, lakini katika dakika ya 120+5, Tielemans alipata penati na kuifunga mwenyewe, akiipa Ubelgiji ushindi wa mabao 3-2 na tiketi ya hatua ya 16 bora.

Ubelgiji sasa itakutana na Marekani katika hatua ya 16 bora baada ya Wamarekani kuifunga Bosnia na Herzegovina mabao 2-0.

Unaweza kusoma;

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *