• Mchungaji Victor Kanyari alifichua kuwa mamake marehemu mke wake wa zamani, Betty Bayo, humpigia simu kila siku akitaka kujua hatua aliyofikia katika kuwachukua watoto wake
  • Akimtetea aliyekuwa mama mkwe wake dhidi ya ukosoaji wa mitandaoni, Kanyari alisisitiza kuwa anaumia sana kutokana na kumpoteza binti yake
  • Katikati ya vita vinavyoendelea vya ulezi wa watoto, mhubiri huyo pia alisema amekuwa akigharamia mahitaji ya kifedha ya watoto hao huku akimwonya binti yake mkubwa kuhusu tabia yake

Mhubiri maarufu wa Nairobi, Mchungaji Victor Kanyari, amefichua kuwa mamake marehemu mke wake wa zamani, Betty Bayo, amekuwa akimpigia simu kila siku kuhusu wajukuu wake.

Mchungaji Kanyari, marehemu Betty Bayo na mama yake.
Mchungaji Kanyari alishiriki kile ambacho mama yake Betty Bayo amekuwa akimuuliza. Picha: Betty Bayo, Prophet Kanyari.
Source: Facebook

Baada ya kifo cha kusikitisha cha mwanamuziki huyo, mamake Bayo aliwataka hadharani baba wa watoto hao, Mchungaji Kanyari, kuchukua hatua za kisheria ili kupata ulezi kamili wa watoto.

Alieleza wasiwasi mkubwa kuhusu mazingira ambayo watoto hao wanaishi kwa sasa chini ya mjane wa Bayo, Tash, na kusema ana azma ya kulinda urithi na mali za wajukuu wake.

Pia soma

Mamake Pasta Kanyari amuenzi bintiye marehemu Starlet Wahu, adai alitumia KSh 26m kumpeleka shule

Kauli zake zilizua hisia mseto mitandaoni, huku watumiaji wa mitandao ya kijamii wakigawanyika kuhusu nia yake halisi na mustakabali wa watoto hao.

Mamake Betty Bayo alimwambia nini Kanyari?

Kanyari na Tash wamekuwa wakipigania ulezi wa watoto hao, jambo ambalo limewafanya marafiki wa Bayo kujitokeza kutoa maoni yao.

Akihubiri kanisani kwake, Kanyari alifichua mazungumzo ambayo amekuwa nayo na aliyekuwa mama mkwe wake.

“Mamake Betty Bayo halali. Ananipigia kila siku akiniuliza, ‘Kanyari, umewachukua watoto?’ Kila siku. Nashangaa watu wa mitandaoni wanamshambulia. Yeye ndiye mwenye uchungu wa kumpoteza binti yake kuliko hata Wakenya,” alisema.

Kanyari pia alisema amekuwa akizungumza na mtoto wake wa kwanza, Sky, na kumwonya aache utovu wa nidhamu ili asiishie kama dada yake marehemu, Starlet Wahu, ambaye aliuawa katika nyumba ya Airbnb.

“Mimi si baba mwenye ubinafsi. Kama ningekuwa baba mwenye ubinafsi, matendo yangu yangeonyesha hivyo. Lakini sivyo. Simu ambayo mtoto anatumia ina thamani ya KSh 160,000. Mimi ndiye nilimnunulia. Nguo zake na kila kitu anachofanya kiko chini ya uangalizi wangu,” alisema.

Tazama video hapa chini:

Haya ni baadhi ya maoni ya watumiaji wa mitandao ya kijamii:

Pia soma

Mzozo wa Kanyari na Tash wazidi makali huku mhubiri huyo akidai shule haimtambui kama baba wa wanawe

@Jerusha Moses alisema:

“Kulea watoto ni zaidi ya kuwapatia mahitaji ya kifedha.”

@Lizzy alisema:

“Huyu mwanaume anaumia.”

@Grant alisema:

“Ukisikiza bila feelings, Kanyari yuko sahihi.”

@Kandie alisema:

“Ni makosa sana kumlinganisha dada yako na binti yako. Bado ni kijana mdogo.”

@Sat Sat alisema:

“Kanyari anafaa kuwachukua watoto ili wawe salama.”

@Njoki wa Njuha alisema:

“Sasa huyo anaongea kama baba wa kweli.”

@Bettie alisema:

“Ukisikiliza bila hisia, kuna jambo la maana analosema.”

Betty Bayo.
Tash, marehemu Betty Bayo na watoto, Sky na Danny. Picha: Betty Bayo.
Source: Facebook

Je, Kanyari alimpeleka Tash mahakamani?

Hivi karibuni Kanyari alipeleka rasmi mahakamani mzozo wa ulezi wa watoto wake kufuatia kifo cha mke wake wa zamani, Betty Bayo, aliyefariki mwezi Novemba mwaka 2025.

Mhubiri huyo alieleza hasira kubwa kutokana na madai kuwa baba wa kambo wa watoto hao, Tash, amekuwa akiwazuia kuzungumza naye kwa simu na pia amekuwa akisimamia vibaya fedha zao.

Akieleza hali hiyo kuwa ni “vita,” Kanyari alichukua hatua za kisheria ili apate fursa ya kuwaona watoto wake na kufungua akaunti huru za benki kwa ajili ya kulinda mapato yao.

Pia soma

Simu Yageuka Chanzo cha Mauti: Mwanafunzi wa Kidato cha Nne Apatikana Amefariki Homa Bay

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *