Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally ni miongoni mwa Watanzania, walioguswa na taarifa iliyotolewa jana Julai 7, 2026, na nyota wa Le Havre AC ya nchini Ufaransa na Timu Tifa ya Tanzania, Mbwana Ally Samatta kuhusu kustaafu kuitumikia Taifa Stars.

Ahmed anasema maumivu wanayosikia Watanzania leo baada ya taarifa ya Samatta, ni kama vile hali watakayokutana nayo Wareno watakaposikia Ronaldo amestaafu Timu ya Taifa au raia wa Argentina watakaposikia Messi anatundika daluga kutumikia taifa lake.

Meneja Habari huyo pia ametolea mfano wa mambo yatakavyokuwa Misri pale watakaposikia tangazo la kustaafu kwa Mo Salah.

Ahmed anasema Samatta ni kielelezo cha mpira wa Tanzania, ambapo timu ikienda kucheza na mataifa mengine, wakimuona mchezaji huyo wanajua kwamba kazini kwao kuna kazi.

Mbwana Samatta ametangaza kustaafu Timu ya Taifa baada ya kuitumikia kwa miaka 15, huku miaka 10 akiwa nahodha.

(Imeandaliwa na @allymufti_tz)

#Samatta #Popa #CaptainDiego

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *