Uhusiano kati ya Mali na Algeria unaimarika baada ya nchi hizo mbili jirani kuzungumza moja kwa moja tangu majira ya kuchipua 2025. Mbali na kufunguliwa tena kwa safari za anga, nchi hizo mbili zimetangaza siku ya Ijumaa, Julai 10, kurejea kwa mabalozi wao katika nafasi zao.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu wa kikanda, Serge Daniel

Mali na Algeria ziliratibu kwa uangalifu tangazo rasmi la mchakato wa kuimarika kwa uhusiano wao. Hapo awali, Algiers, katika taarifa, ilitangaza kufunguliwa tena anga yake kwa safari za anga ya Mali kuanzia siku ya Ijumaa.

Bara tu baada ya hili, Bamako ilitoa matangazo mawili: kufunguliwa tena kwa anga yake kwa ndege zote za kiraia na kijeshi zinazofanya kazi kwenda na kurudi Algeria. Mali pia ilitangaza kurejea kwa balozi wake nchini Algeria.

Kisha Algeria, nayo, ilitangaza kurejea kwa balozi wake huko Bamako.

Ishara ya utulivu

Matangazo haya ni ushahidi wa kuanzishwa kwa uhusiano kati ya nchi hizo mbili. Tangu jeshi la Mali lilipochukua madaraka kufuatia mapinduzi mawili ya mwaka 2020 na 2021, uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulizorota. Mgogoro huo ulifikia kilele chake miaka minne baadaye kwa kuangushwa kwa ndege isiyo na rubani ya Mali karibu na mpaka kati ya nchi hizo mbili.

Waalgeria walidai kuwa ndege hiyo isiyo na rubani ilikiuka anga yao. Mali, kwa upande wake, ilibainisha kuwa ndege hiyo isiyo na rubani ilikuwa ndani ya eneo lake.

Kupungua huku kwa mvutano kunakuja huku hali ya usalama ikizidi kuzorota kaskazini mwa Mali, ambapo muungano wa wapiganaji wa wanajihadi na waasi wanaotaka kujitenga uliteka udhibiti wa Kidal, mji ulioko katika eneo linalopakana na Algeria, miezi miwili iliyopita.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *