- Canada imechapisha masharti yake mapya ya kuingia nchini kwa mwaka 2026, yakieleza ni raia wa mataifa gani wanaoweza kusafiri bila kuhitaji viza ya kawaida ya wageni
- Kundi dogo la wasafiri linastahili msamaha kamili wa kutohitaji viza ya wageni wala Kibali cha Kielektroniki cha Kusafiri (Electronic Travel Authorisation – eTA)
- Zaidi ya nchi 50 zinastahili kutumia mfumo wa eTA, ambao unawahusu tu wasafiri wanaosafiri kwa ndege na hauhitajiki kwa wanaoingia kwa njia ya nchi kavu au baharini
Mwandishi wa TUKO.co.ke Japhet Ruto ana zaidi ya miaka minane ya uzoefu wa kuripoti kuhusu masuala ya fedha, biashara na teknolojia, akitoa uchambuzi kuhusu mwenendo wa uchumi wa Kenya na dunia.

Source: Facebook
Canada imechapisha maelezo kamili ya masharti yake mapya ya kuingia nchini kwa mwaka 2026, ikifafanua ni mataifa gani yanaweza kutembelea nchi hiyo bila kuhitaji viza ya kawaida ya wageni.
Idara ya Uhamiaji, Wakimbizi na Uraia ya Canada (Immigration, Refugees and Citizenship Canada – IRCC) ilitoa mwongozo huo kupitia tovuti yake rasmi, ikiwagawa wasafiri kulingana na uraia wao na njia ya usafiri ili kufafanua nyaraka zinazohitajika kabla ya kufika kwenye mpaka wa Canada.

Pia soma
Magazeti ya Kenya: Utafiti wasema huenda kura ya urais ya 2027 ikakosa mshindi raundi ya kwanza
Nani anastahili msamaha kamili?
Kundi dogo la wasafiri halitahitajika kuwa na viza ya kawaida ya wageni wala Kibali cha Kielektroniki cha Kusafiri (eTA).
Kundi hilo linajumuisha:
- Wenye pasipoti za kidiplomasia.
- Wahudumu wa ndege za usafirishaji wa kibiashara wanaokidhi masharti maalumu ya kiutendaji.
Raia wa Ufaransa wanaosafiri moja kwa moja kutoka eneo la Saint-Pierre-et-Miquelon pia wamejumuishwa katika kundi hili la msamaha kamili.
Wakazi wa kudumu halali wa Marekani (US lawful permanent residents) wanatakiwa kuwa na kadi halali ya ukaazi wa kudumu (Green Card) au uthibitisho mwingine halali wa hadhi yao nchini Marekani pamoja na pasipoti halali ya nchi yao.
Raia wa Marekani wanatakiwa kuwa na pasipoti halali.
Ni nchi zipi zinastahili kuingia kwa eTA?
Kundi kubwa zaidi la mataifa linaweza kuingia Canada bila viza ya kawaida, mradi wasafiri kwa ndege na wawe wamepata kibali halali cha eTA kabla ya kuondoka.
Muhimu kutambua ni kwamba wasafiri kutoka nchi hizi wanaoingia Canada kwa njia ya nchi kavu au baharini hawahitaji eTA.
“Baadhi ya wasafiri lazima wawe na eTA kabla ya kusafiri kwenda Canada,” ilisema IRCC.
Nchi ambazo raia wake wanastahili kutumia mfumo huu ni:
Andorra, Australia, Austria, Bahamas, Barbados, Belgium, Brunei Darussalam, Bulgaria, Chile, Croatia, Cyprus, Czech Republic, Denmark, Estonia, Finland, France, Germany, Greece, Hungary, Iceland, Ireland, Israel, Italy, Japan, Republic of Korea, Latvia, Liechtenstein, Lithuania, Luxembourg, Malta, Monaco, Netherlands, New Zealand, Norway, Papua New Guinea, Poland, Portugal, Qatar na Romania.
Kwa wenye pasipoti za kielektroniki (electronic passports) pekee, nchi zinazostahili pia ni:
Samoa, San Marino, Singapore, Slovakia, Slovenia, Solomon Islands, Spain, Sweden, Switzerland, Taiwan, United Arab Emirates, United Kingdom na Vatican City State.
Wasafiri ambao nchi zao hazipo katika orodha hizo kwa ujumla wanapaswa kuomba viza ya kawaida ya wageni wa Canada kabla ya kupanga safari yao.
Nani anastahili eTA kwa masharti maalumu?
IRCC pia imeorodhesha kundi jingine la nchi ambazo kwa kawaida zinahitaji viza, lakini raia wake wanaweza kustahili kupata eTA iwapo watatimiza masharti maalumu.
Wasafiri hao lazima watimize vigezo vingine, kama vile kuwa na vibali halali vya kusafiri vilivyotolewa na mamlaka maalumu za nchi nyingine na wasafiri kwa ndege pekee ili wanufaike na utaratibu huo.

Pia soma
Magazeti ya Kenya: Linda Mwananchi yaweka tarehe ya kuzinduliwa kwa safari ya Sifuna kwenda Ikulu
Mfumo huo mpya unawapa wasafiri uelewa mpana zaidi wa nyaraka wanazohitaji kabla ya kupanga safari, na ndio maelezo ya kina zaidi yaliyowahi kutolewa hadharani kuhusu mfumo wa Canada wa viwango tofauti vya masharti ya kuingia nchini.
Nani anaweza kutembelea Marekani bila viza?
Katika habari nyingine, raia wa mataifa 42 yaliyokubaliwa wanaweza kusafiri kwenda Marekani kwa hadi siku 90 bila kuhitaji viza kupitia Mpango wa Marekani wa Kuondoa Hitaji la Viza (US Visa Waiver Programme).
Ingawa muhuri wa viza hauhitajiki, wasafiri lazima wawe na kibali halali cha Electronic System for Travel Authorisation (ESTA) kabla ya kupanda ndege.
Mpango huo hauwahusu tena raia wa nchi zilizo kwenye Visa Waiver Programme (VWP) ambao pia ni raia wa Cuba, Iran, Iraq, Korea Kaskazini, Sudan au Syria.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke
