Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Argentina ya Lionel Messi itamenyana na England katika nusu fainali ya Kombe la Dunia Jumatano, huku Uhispania ikisubiri mshindi baada ya kuzima ndoto za Ufaransa za kutwaa ubingwa wa tatu wa dunia.

Mchezo huo unakutanisha mataifa mawili makubwa ya soka duniani, lakini pia unabeba historia ndefu ya uhasama wa kisiasa kati ya nchi hizo.

Argentina ya kocha Lionel Scaloni inataka kuwa timu ya kwanza tangu Brazil mwaka 1962 kutwaa Kombe la Dunia mara mbili mfululizo. Mafanikio hayo pia yatakuwa hitimisho la kipekee kwa Lionel Messi.

Nahodha huyo mwenye umri wa miaka 39 anaongoza orodha ya wafungaji akiwa na mabao manane. Aliiongoza Argentina kutwaa Kombe la Dunia nchini Qatar mwaka 2022 katika kile kilichoonekana kuwa mashindano yake ya mwisho, lakini amerejea tena na ameendelea kuwa tegemeo la timu hiyo.

Messi amefunga katika ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Cape Verde na Misri, akiisaidia Argentina kutinga hatua ya nusu fainali.

Hata hivyo, Argentina, mabingwa mara tatu wa dunia, sasa wanakabiliwa na mtihani mkubwa zaidi dhidi ya

Uingereza
Uingereza AP Photo/Rebecca Blackwell – Rebecca Blackwell

ambayo licha ya kutong’ara katika baadhi ya mechi, imeendelea kupata matokeo.

Harry Kane na Jude Bellingham wamefunga mabao 12 kati ya 13 ya England katika mashindano haya.

Timu hizo zitakutana kwa mara ya kwanza katika mechi ya mashindano tangu Kombe la Dunia la mwaka 2002.

Kocha wa England Thomas Tuchel amesema hahisi presha ya ziada licha ya ukubwa wa pambano hilo.

“Sihisi mzigo. Tutakuwa na msisimko na wasiwasi, lakini hilo ni jambo la kawaida. Ninachopenda ni kuona wachezaji wana ushindani, wana hamu na wana shauku ya kucheza mechi hii,” alisema Tuchel.

Mchezaji wa Uingereza Jude Bellingham akishangilia baada ya kufunga bao la pili dhidi ya Norway katika mechi ya robo fainali ya Kombe la Dunia kati ya Norway na Uingereza huko Miami Gardens, Florida, siku ya Jumamosi, Julai 11, 2026. (Picha ya AP/Lynne Sladky)
Mchezaji wa Uingereza Jude Bellingham akishangilia baada ya kufunga bao la pili dhidi ya Norway katika mechi ya robo fainali ya Kombe la Dunia kati ya Norway na Uingereza huko Miami Gardens, Florida, siku ya Jumamosi, Julai 11, 2026. (Picha ya AP/Lynne Sladky) AP Photo/Lynne Sladky – Lynne Sladky

Pia amethibitisha kuwa kiungo Declan Rice amepona maradhi na yuko tayari kuanza mchezo.

Argentina na England zina historia ndefu katika Kombe la Dunia. Mwaka 1986, Diego Maradona aliiongoza Argentina kuifunga England mabao 2-1 kwa mabao mawili, likiwemo maarufu la “Hand of God”.

Miaka 12 baadaye, David Beckham alitolewa kwa kadi nyekundu kabla Argentina haijashinda kwa mikwaju ya penalti.

Pambano hilo pia lafanyika huku kukiwa na historia ya mgogoro wa Visiwa vya Falkland, vinavyojulikana kwa Kihispania kama Malvinas.

Hata hivyo, Scaloni amesema mechi hiyo ni ya soka pekee na haipaswi kuchanganywa na siasa.

Uhispania ilitinga fainali Jumanne baada ya kuifunga Ufaransa mabao 2-0. Mikel Oyarzabal alifunga bao la kwanza kwa penalti kabla Pedro Porro kuongeza la pili. Ushindi huo ulimaliza safari ya kocha Didier Deschamps katika Kombe la Dunia.

Kocha wa Uhispania Luis de la Fuente alisema mafanikio hayo yametokana na kuamini mpango walioanza karibu miaka minne iliyopita. Aliwasifu wachezaji wake kwa kujituma, mshikamano na vipaji vyao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *