Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Félix-Antoine Tshisekedi ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo, Patrice Emery Lumumba, kufuatia kifo cha mtoto wa kiongozi huyo, Roland-Gilbert Okito Lumumba.

Roland-Gilbert, ambaye ni mtoto wa mwisho wa Patrice Emery Lumumba, alifariki dunia jijini Kinshasa, akiwa na umri wa miaka 67, baada ya kuugua.

Mtaalamu huyo wa usanifu wa majengo ambaye pia, amewahi kuhudumu kama mbunge wa zamani nchini DRC, atakumbukwa kwa jitihada zake za kutafuta ukweli kuhusu kifo cha baba yake, Patrice Lumumba, ambaye aliuawa mwaka wa 1961.

Kifo chake kinakuja wakati kesi za mauaji ya Patrice Lumumba zikiwa bado zinaendelea nchini Ubelgiji.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *