Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, siku tano baada ya maporomoko makubwa ya ardhi katika eneo la mgodi wa Rubaya katika jimbo la Kivu Kaskazini, idadi halisi ya vifo bado haijulikani. Kulingana na mamlaka za ndani, maporomoko ya ardhi yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 200. Hata hivyo, mashirika ya kiraia katika eneo la Masisi yanataja idadi ya vifo vya watu karibu 400.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Eneo la Rubaya liko zaidi ya kilomita 70 magharibi mwa Goma, katika eneo gumu kufikika la DRC. Mtandao wa simu umezimwa kwa siku kadhaa, na taarifa hutolewa na waendesha pikipiki wanaosafiri katika eneo hilo.

Ni vigumu kubaini idadi kamili ya vifo, ikizingatiwa kwamba mamlaka za ndani zinaripoti vifo vya watu wasiopungua 200 huku mashirika ya kiraia yakiripoti zaidi ya vifo 400. Miili mia kadhaa bado haipo, imefukiwa kwenye matope, kulingana na mwakilishi wa mashirika ya kiraia. Kulingana kiongozi huyu, itachukua muda kukusanya orodha ya waathiriwa.

Kama ukumbusho, sehemu ya kilima ilianguka siku ya Jumatano, Januari 28, baada ya mvua kubwa katika eneo la uchimbaji madini la Luwowo, lililoko ndani ya eneo la uchimbaji madini la Rubaya, ikifuatiwa na maporomoko mengine ya ardhi asubuhi iliyofuata.

Mashirika yasiyo ya kiserikali ya haki za binadamu yanalaani ukweli kwamba maelfu ya wachimbaji madini wanafanya kazi kila siku katika mashimo ya Rubaya chini ya hali hatarishi na bila hatua za usalama. Shughuli hii hutoa mapato kwa familia nyingi za wenyeji, ingawa mishahara kwa ujumla ni ya chini sana. Eneo hilo liko katika eneo linalodhibitiwa na kundi lenye silaha la AFC-M23.

Mwaka mmoja uliopita, serikali ya Kinshasa ililiainisha kama eneo jekundu, ikipiga marufuku shughuli zote za uchimbaji madini na biashara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *