Baada ya vitisho, wakati wa mazungumzo unawadia. Iran na Marekani zitaanza mazungumzo ya nyuklia, labda mapema mwishoni mwa wiki hii. Mjumbe wa Marekani Steve Witkoff na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi wanatarajiwa kukutana siku ya Ijumaa hii, Februari 6, huko Istanbul, Uturuki. Mwishoi mwa wiki iliyopita, Donald Trump alionyesha imani katika uwezekano wa kufikia makubaliano na Tehran.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Makubaliano ambayo Donald Trump anaonekana kuyatarajia huenda yasifanane sana na yale yaliyosainiwa mwaka wa 2015 na Barack Obama. Baada ya kuibua dalili za kuingilia kijeshi na kutuma meli kadhaa kwenda Ghuba, rais wa Marekani yuko katika hali ya kutumia nguvu dhidi ya mamlaka ya Iran iliyodhoofishwa na upinzani wa ndani.

Kwa hivyo, Donald Trump anakusudia kutoa makubaliano muhimu katika nyanja kadhaa: kukomesha usaidizi wa Iran kwa wawakilishi wake wenye silaha katika eneo hilo, kama vile Hezbollah na Houthi, kusitishwa kabisa kwa urutubishaji wa uranium, na kusitisha mpango wake wa makombora ya balestiki.

Haikubaliki, inajibu Tehran, ambayo bila shaka haikusudii kwenda mbali zaidi ya mwaka 2015. Wakati huo, nchi ilikubali mpango mpana wa ufuatiliaji kutoka kwa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA).

Makubaliano “yanawezekana,” kulingana na wanadiplomasia wa Iran

“Rais Trump anasema ‘hakuna silaha za nyuklia,’ na tunakubaliana kabisa na hoja hiyo. (…) Bila shaka, kwa upande mwingine, tunatarajia kuondolewa kwa vikwazo. Kwa hivyo makubaliano haya yanawezekana.” “Tusizungumzie mambo yasiyowezekana,” Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi alibainisha kwenye CNN siku ya Jumapili, Februari 1. Iran pia imekataa kujadili uwezo wake wa ulinzi na makombora ya balestiki.

Siku ya Jumanne, Februari 3, Rais wa Iran Masoud Pezeshkian alitangaza kwamba alimpa Waziri wake wa Mambo ya Nje jukumu la kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani, “mradi tu mazingira yanayofaa yawepo.” “Nimemwomba Waziri wangu wa Mambo ya Nje, mradi tu kuwe na mazingira yanayofaa, bila vitisho au madai yasiyo na msingi, kufanya mazungumzo ya haki … ndani ya mfumo wa maslahi yetu ya kitaifa,” amesema kwenye X.

Mnamo mwaka 2018, Donald Trump alielezea makubaliano ya nyuklia ya Iran ya 2015 kama “ya kutisha,” “mabaya zaidi ambayo Marekani imewahi kusaini.” Rais wa Marekani pia aliishutumu Tehran kwa kutoheshimu ahadi zake, bila kutoa ushahidi wowote. Akishawishiwa na Israel, hatimaye alitangaza kujiondoa kwa Marekani kutoka kwa makubaliano hayo.

Steve Witkoff anatarajiwa kukutana na Benjamin Netanyahu Kwa kusubiri mazungumzo yanaendelea, na mjumbe maalum wa Marekani kwa eneo hilo, Steve Witkoff, anatarajiwa nchini Israel mnamo Februari 3. Anatarajiwa kukutana na Benjamin Netanyahu na Mkuu wa majeshi, Eyal Zamir, ambaye amerejea kutoka zirani Washington. Nchini Marekani, aliwasilisha mipango ya ulinzi na mashambulizi ya Israel iwapo vita vitatokea, kulingana na tovuti ya Marekani ya Axios. Kwa Israel, nafasi za kufanikiwa kwa mazungumzo ya sasa ni ndogo. Dhana iliyopo ni ile ya shambulio la Marekani.

Waziri Mkuu wa Israel alizungumzia vitisho hivi katika hotuba yake mbele ya Bunge siku ya Jumatatu, Februari 2, anaripoti mwandishi wa RFI huko Jerusalemu, Frédérique Misslin, akitangaza kwamba taifa la Kiyahudi lilikuwa “tayari kukabiliana na hali zote.” Benjamin Netanyahu anajaribu kumshawishi Donald Trump kwamba Iran lazima isimamishe urutubishaji wa uranium, mpango wake wa makombora ya balestiki, na usaidizi wake kwa makundi yenye silaha katika eneo hilo. Ikiwa itafanyika, mkutano kati ya Marekani na Iran huko Istanbul siku ya Ijumaa, Februari 6, utakuwa wa kwanza tangu vita vya siku 12 vilivyoanzishwa na Israel dhidi ya Iran mnamo mwezi Juni 2025.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *