• Mke wa mtangazaji wa habari wa BBC, Waihiga Mwaura, Joyce Omondi, walihiriki video ya kupendeza wakiwa na mwanao mchanga
  • Familia ya Waihiga, ambao hupenda kuweka maisha yao ya ndoa kuwa ya faragha, walitangaza kuwa walibarikiwa na mtoto wa kiume mwaka 2025
  • Wanandoa hao waliofunga ndoa mwaka 2015 waliwaacha mashabiki wakijiuliza kwa miaka kadhaa ni lini wangepata mtoto wao wa kwanza

Mtangazaji wa habari wa BBC Waihiga Mwaura na mkewe Joyce Omondi walipata mtoto wa kiume mwaka 2024.

Joyce Omondi (picha kuu), upande wa juu (Joyce akiwa na mwanae).
Joyce Omondi akifurahia muda na mwanawe. Picha: Joyce Omondi.
Source: Instagram

Wanandoa hao walificha habari hiyo kwa muda na walitangaza rasmi mwezi Desemba 2025.

Waihiga Mwaura ana watoto wangapi?

Mtangazaji huyo na mkewe walifunga ndoa mwaka 2015, na mashabiki waliokuwa na udadisi walikuwa wakiwauliza mara kwa mara ni lini wangepata mtoto wao wa kwanza.

Baadhi ya mashabiki walimtaka Joyce asijibu maswali aina hiyo yasiyo na hisia.

Wakenya wengine walieleza kwamba walikuwa wakiwaombea wanandoa hao wapate baraka ya mtoto.

Mwaka 2022, Joyce aliapa kuweka mambo ya ndoa yake na Waihiga kuwa ya faragha, akisisitiza kuwa ameolewa na mwanaume mmoja tu.

Pia soma

Wanandoa Washuhudia Kwa Machozi Mungu Alivyowajalia Mtoto Baada ya Miaka 30

Mtangazaji huyo wa kipindi cha Rauka alibainisha kuwa alifanya agano kati yake, Mungu na Waihiga, jambo lililomfanya asitake kuwahusisha watu wengine katika uhusiano wao.

Mtangazaji huyo wa habari alifichua furaha ya familia yake mwezi Desemba, akiongeza kuwa mioyo yao ilikuwa imejaa shukrani.

“Mwaka jana, Mungu alibariki familia yetu kwa zawadi ya thamani sana. Kila siku tangu hapo imekuwa ushuhuda wa wema na uaminifu wa Mungu. Tumefurahia kipindi hiki kipya kizuri cha maisha yetu, kwa utulivu tukifurahia kila wakati. Mioyo yetu imejaa sana, na tunashukuru kushiriki furaha inayochanua nyumbani kwetu. Krismasi Njema kutoka kwa familia ya Waihiga,” aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Joyce alishiriki mkusanyiko wa matukio yake ya hivi karibuni kwenye Instagram, na akatoa taarifa adimu kuhusu mwanawe mdogo.

Mke wa mtangazaji huyo na mwanawe walionekana wakicheza pamoja katika video fupi.

Mtoto huyo alionekana amekua zaidi kwenye video hiyo.

Joyce alionekana akimshikilia mikono mwanawe walipokuwa wakicheza pamoja na akaandika maelezo yafuatayo:

“Mtalaika wetu mchanga anakua kwa kasi sana.”

Je, Joyce alikanusha uvumi wa ujauzito?

Katika habari nyingine, Joyce aliwahi kukanusha uvumi wa ujauzito baada ya mashabiki wake kudai kwamba alionekana kuwa mjamzito.

Pia soma

Wajackoyah Asema Raila Aliondoka Katika Serikali Mpana Kabla Ya Kufa, Adai Ndiye Mrithi Wake

Mwimbaji huyo wa nyimbo za injili alishiriki picha yake akiwa amevaa gauni refu la rangi ya machungwa lenye michoro ya bluu, na watu wakaanza kumpongeza.

Joyce alikanusha uvumi huo kwa ustaarabu, akiwakumbusha mashabiki wake kuwa wakati wa Mungu ndio bora zaidi.

Joyce Omondi akiwa amevalia vazi jeusi kabisa na kiakisi.
Joyce Omondi na mumewe walimkaribisha mtoto wa kiume mwaka wa 2024. Picha: Joyce Omondi.
Source: Instagram

Baadhi ya watu walimwambia kwamba walikuwa wakimwombea siku moja apate furaha ya kuwa mama.

Familia ya Waihiga siyo pekee waliokumbana na maswali ya udadisi kutoka kwa mashabiki.

Mke wa Bien Baraza, Chiki Kuruka, mwezi Desemba aliwaomba Wakenya waache kuuliza maswali yasiyo na hisia.

Chiki alifichua kuwa mara nyingi huulizwa ni lini yeye na mumewe watapata mtoto, na wakati mwingine hujibu kulingana na uhalisia wa mtu anayemuuliza.

Aliongeza pia kuwa watu wengine waliwahi kumwambia mumewe aoe mwanamke mwingine ambaye angeweza kumzalia mtoto.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *