
Uhusiano kati ya Algiers na Niamey ulizorota mwezi Aprili 2025 wakati Algiers ilipotangaza kuwa imedungua ndege isiyo na rubani ya Mali. Nchi hizo tatu za ESA kisha ziliwaita mabalozi wao kwa ajili ya mashauriano. Algeria pia iliwaondoa wawakilishi wake. Kwa Niamey, hali sasa imebadilika.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Mgogoro wa kidiplomasia umekwisha. Mabalozi wanarudi kwenye nafasi zao: Balozi wa Niger huko Algiers alifanya hivyo siku ya Alhamisi, Februari 12, 2026. Balozi wa Algeria huko Niamey atafanya vivyo hivyo, kufuatia uamuzi wa rais Abdelmadjid Tebboune. Kulingana na taarifa ya Algeria, hatua hii inaonyesha umuhimu mkubwa ambao mkuu wa nchi ya Algeria anaupa katika kuimarisha uhusiano na Niger. Algiers inaendelea, inapaswa kukuza kuanza tena kwa mazungumzo katika ngazi ya juu na utekelezaji wa miradi ya kimkakati.
Hivi majuzi, majirani hao wawili wameonyesha dalili kadhaa za kudorora kwa mahusiano yao. Wiki iliyopita, mbele ya waandishi wa habari wa ndani, Abdelmadjid Tebboune alimwalika Abdourahamane Tiani kwa ziara rasmi huko Algiers. Mwishoni mwa mwezi Januari, ujumbe mkubwa wa Algeria, ukiongozwa na Waziri wa Hidrokaboni, Mohamed Arkab, ulitembelea Niamey. Walijadili, miongoni mwa mambo mengine, mradi wa eneo la mafuta la Kafra kaskazini mwa Niger na mradi wa Bomba la gesi la Trans-Saharan.
Ingawa uhusiano umerejea tena upande wa Niger, bado Bamako na Algiers hawajaweza kufanya chochote kufufua mahusaino yao. Mamlaka ya mpito ya Mali inaishutumu Algeria kwa kuingilia masuala ya Mali na kuunga mkono makundi ya “magaidi”.