Gyokeres ameanza kuwalizaGyokeres ameanza kuwaliza

ENGLAND: Mabao mawili aliyofunga dhidi ya ‘Spurs’ yanamfanya mshambuliaji wa Arsenal, Viktor Gyokeres kuwa wenye mabao mengi kuliko mchezaji yoyote Ligi Kuu ya England kwa mwaka 2026 katika michuano yote.

Gyokeres amefikisha mabao 8, akifuatiwa na Joao Pedro wa Chelsea, Anthony Gordon wa Newcastle wenye 7, Igor Thiago wa Brentford, Crysencio Summerville, Antoine Semenyo wana 6. Kwa Ujumla amefikisha mabao 10 ya Ligi Kuu.

Gyokeres amefunga mabao 4 kwenye michezo mitano ya mwisho, na mabao 7 amefunga kwenye michezo 12 ya michuano yote wanayoshiriki Arsenal.

Arsenal wameendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu England wakiwa na pointi 61 na mchezo mmoja mbele. Manchester City wanafuata wakiwa na pointi 56.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *