- Mfanyabiashara wa Nairobi mwenye umri wa miaka 27 anaendelea kupigania maisha yake hospitalini baada ya kudaiwa kumwagiliwa maji moto na mpenzi wake usiku wa mapema wa Siku ya Wapendanao
- Steve Godia alipata majeraha ya moto yanayokadiria 21% kwenye uso, shingo, masikio, macho, nyuma ya kichwa, na sehemu ya mgongo baada ya shambulio hilo alilokuwa amelala
- Akizungumza na TUKO.co.ke, wanandoa hao walikuwa wametatua mzozo wa awali, na Steve alidhani kila kitu kiko sawa kabla ya kulala. Mshukiwa pia anadaiwa kuiba KSh 318,000 kutoka kwa mwathirika baada ya shambulio
Familia ya mfanyabiashara mmoja wa Nairobi sasa inatafuta haki baada ya kudaiwa kushambuliwa na mpenzi wake kwa maji moto na kuachwa na majeraha mabaya.njuries.

Source: TikTok
Kwa wiki kadhaa sasa, Steve Godia mwenye umri wa miaka 27 amekuwa hospitalini baada ya kuungua kwa asilimia 21 usoni mwake, ikiwa ni pamoja na shingo, masikio na macho, sehemu ya nyuma ya kichwa na upande wa mgongo.
Akizungumza kwa uchungu, dadake Brendah alisema kuwa mateso ya ndugu yake yalianza usiku wa Siku ya Wapendanao baada ya mabishano na mpenzi wake.
Wote walitatua mzozo huo, na alifikiri kuwa uhusiano wao uko sawa.
“Alithibitisha pia kwamba hakukuwa na shida tena. Baada ya hapo, alizima TV kupumzika na kisha kuamua kulala kidogo,” Brendah alieleza.
Hata hivyo, alipokuwa amelala, mpenzi wa Steve anadaiwa kumwagilia maji moto, na kumuacha akiwa na majeraha mazito.
“Baada ya kumshambulia, alihepa na simu zake, akimuacha peke yake katika hali hatari. Zaidi ya hayo, aliiiba pia KSh 318,000. Hii ilikuwa pesa ndugu yangu alipokea kutoka kwa wateja wake kununua vifaa na kuvituma kama kawaida. Kawaida hununua vifaa kutoka Eastleigh na kuvituma kwa wateja wake Somalia na sehemu nyingine za nchi,” alisema ndugu wa mwathirika.
Brendah alisema kuwa kulingana na taarifa za M-Pesa za ndugu yake, KSh 318,000 zilipelekwa kwenye namba ya mpenzi wake kabla ya yeye kukimbia.
Mbali na hali hatari ya kiafya, mwathirika sasa pia analilia kuhusu hasara kubwa ya kifedha aliyopatiwa na mshukiwa.
“Amekuwa akifanya biashara hii kwa takribani miaka mitano, na wateja wake wanamwamini kwa sababu amekuwa mwaminifu. Kwa bahati mbaya, siku ile ile tukio lilipotokea, KSh 318,000 zilitumwa kutoka simu ya ndugu yangu kwenda kwenye simu yake, kulingana na taarifa ya M-Pesa. Hii imeongeza ugumu wa hali hiyo kwa sababu, mbali na kushughulikia majeraha makubwa na mshtuko, sasa pia anakabiliwa na hasara kubwa ya kifedha na jukumu la kueleza kwa wateja wake kilichotokea,” alisema dadake.

Pia soma
Wesley Fofana: Nyota wa Chelsea afunguka sababu ya kulia mechi yao ya Kombe la Carabao na Arsenal
Familia ya Steve inatafuta msaada na haki
Brendah alishiriki picha zinazoonyesha kuwa ndugu yake alibaki hana sura ya awali kutokana na majeraha ya moto.
Amekuwa akipokea matibabu kwa karibu wiki mbili, na bili ya hospitali inaendelea kuongezeka, ikileta mzigo kwa familia huku pia wakitafuta haki.
Hadi Jumanne, Februari 24, bili ilikuwa KSh 106,000, na familia sasa inatafuta msaada kutoka kwa wafuasi na Wsamaria kulipa gharama hizo huku Steve akiendelea kupatiwa matibabu.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke
