Mpina

Chanzo cha picha, ACT

Maelezo ya picha, Mpina

ACT Wazalendo imemuidhinisha rasmi bwana Luhaga Mpina kuwa mmoja wa wagombea wa Urais atakayechuana na Rais Samia Suluhu Hassan wa CCM kwenye uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu.

Uamuzi huo umefikiwa na Halmashauri Kuu ya ACT wazalendo jijini Dar es Salaam, ambayo ilipendekeza majina mawili, Aaron Kalikawe na Luhaga Mpina.

Majina hayo yaliyopendekezwa yaliwasilishwa kwa Mkutano Mkuu Taifa kwa ajili ya kupigiwa kura, ambapo katika mkutano huo, Mpina alichaguliwa kwa kishindo kwa kupata kura 559 sawa na asilimia 92.3 ya kura zote 610 zilizopigwa.

Luhaga Mpina amemshinda Mgombea mwenzake Kalikawe aliyepata kura 46 sawa na asilimia 7.7 na sasa atapeperusha bendera ya ACT katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, mgombea mwenza akiwa Bi. Fatma Ferej.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *