Miezi minane baada ya kusainiwa kwa makubaliano ya amani kati ya DRC na Rwanda chini ya usimamizi wa Marekani mnamo Juni 27, matokeo yanachelewa kufikiwa. Kulingana na ripoti ya tathmini iliyochapishwa siku ya Jumanne, Machi 3, huko Kinshasa na shirika linalojihusisha na Mikataba ya Amani ya Afrika, Mkataba wa Washington umetekelezwa kwa 23%, na kuwaacha raia katika hali mbaya ya kibinadamu.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Ili kuzuia kuanguka kabisa kwa Mkataba wa Washington, ripoti hiyo inaitaka Marekani kuongeza shinikizo la kidiplomasia kwa miji mikuu yote miwili (Kinshasa na Kigali). Inaitaka DRC kuharakisha operesheni dhidi ya FDLR na inaitaka Rwanda kuanza kuondoa hatua kwa hatua hatua za ulinzi mpakani.

Pande zote mbili zinapendekezwa kuanza tena, bila kuchelewa, mikutano ya mifumo ya pamoja ya ufuatiliaji, ambayo kwa sasa imesimama.

Kulingana na shirika hilo, mifumo ya utekelezaji iko katika hali ya “kuzorota.” Kwa jumla ya alama 10, vipaumbele muhimu kama vile ulinzi wa raia, misaada kwa watu walio katika mazingira magumu, na kurejea kwa watu waliokimbia makazi yao vinapata alama mbaya ya 2.5/10.

Ripoti inabainisha kwamba mizizi ya mgogoro huo bado haijabadilika licha ya ahadi zilizotolewa chini ya usimamizi wa Marekani. Vikwazo kadhaa vikubwa vinazuia kupungua kwa mzozo:

Uhasama mkali: Mapigano yanaendelea katika maeneo kadhaa ya mashariki mwa DRC.

Hali ilivyo katika masuala ya kijeshi: Kushindwa kwa Kinshasa kuwazuia au kuwaangamiza waasi wa FDLR na Kigali kudumisha hatua za ulinzi za Rwanda kunazuia utekelezaji wa vifungu vya usalama.

Mgogoro wa kibinadamu: Upatikanaji wa maeneo ya migogoro kwa mashirika ya kutoa misaada bado unazuiwa na pande zinazopigana.

Diplomasia, mwanga pekee wa matumaini?

Ingawa hali bado ni tete katika maeneo mbalimbali mshariki mwa DRC, ripoti inabainisha maendeleo makubwa katika duru za kidiplomasia. Upatanishi wa kikanda na shinikizo la kimataifa vimewezesha:

Tangazo la msaada wa Ulaya wenye thamani ya zaidi ya euro milioni 81 .

Vikao muhimu mbele ya Bunge la Marekani.

Vikwazo dhidi ya wale wanaoshutumiwa kwa kuharibu mchakato wa amani.

Hata hivyo, kulingana na shirika linalojihusisha na Mikataba ya Amani ya Afrika, juhudi hizi za kidiplomasia hazitoshi kubadilisha hali kwa watu wa mikoa ya Kivu Kaskazini na Ituri.

Ripoti inahitimisha kuwa wakati wa kutangaza nia umekwisha, na sasa ni kwa kila mhusika kuongeza uwajibikaji ili kubadilisha hati hii kuwa amani inayoonekana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *