Nchini Guinea, serikali imetangaza usiku wa Ijumaa, Machi 1, kuvunjwa kwa vyama arobaini vya siasa, vikiwemo vitatu vikubwa zaidi: chama cha RPG, kinachoongozwa na rais wa zamani Alpha Condé; chama cha UFDG, kinachoongozwa na Waziri Mkuu wa zamani Cellou Dalein Diallo; na chama cha UFR, kinachoongozwa na Waziri Mkuu wa zamani Sidya Touré. Kulingana na sheria hiyo, vyama hivi vya siasa vimevunjwa kwa kutofuata sheria mpya ya Guine iliyopitishwa mnamo Septemba 21, 2025.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Tangazo hilo lilitolewa kwenye televisheni ya umma. Majina ya vyama arobaini vya siasa vilivyovunjwa yalisomwa na kurushwa hewani. Sheria hiyo, iliyosainiwa Machi 6 na Ibrahima Kalil Condé, Waziri wa Mambo ya Ndani, inabainisha kuwa vyama hivi haviruhusiwi tena kushiriki katika shughuli za kisiasa.

“Kuvunjwa huku kunahusisha kupoteza mara moja utu wa kisheria na hadhi ya vyama vya siasa husika,” hati rasmi inasema. Serikali pia ilitangaza kunyang’anywa mali zote za vyama hivi kote Guinea, anaripoti mwandishi wetu huko Conakry, Moktar Bah.

Uamuzi huu, ambao viongozi wa kisiasa wanahofia, umekuja kama mshtuko, kwani vyama vya siasa vilikuwa na hadi Mei 25 kusasisha sheria zao na kanuni za ndani, kufanya makongamano ya kufuata sheria, na kutoa uthibitisho wa makao yao makuu katika kila mkoa wa nchi.

Sheria hiyo inakuuja huku Guinea ikijiandaa kwa uchaguzi wa wabunge, wa serikali za mitaa, na wa maseneta mnamo Mei 24.

“Hatua itasababisha hali kuwa mbaya zaidi”

Majibu kutoka kwa upinzani wa kisiasa kufuatia tangazo hili la serikali ya Guinea yalikuwa ya haraka, haswa kutoka kwa UFDG, chama cha kiongozi Cellou Dalein Diallo. Kwa Souleymane Souza Konaté, msemaji wa chama hiki, anasema kufutwa kwa vyama vya siasa ni “kunyamazisha kabisa sauti zote zinazoikosoa serikali.”

“Tangu jana usiku, sauti zote zinazoikosia serikali zimevukwa nchini Guinea. Kuvunjwa kwa vyama vya siasa vinavyowakilisha watu wa Guinea—vile vinavyojumuisha karibu 95% ya wananchi wenzetu—kunaunda kitendo cha mwisho cha sitofahamu ya kisiasa ambayo lengo lake ni kuanzishwa kwa chama kimoja nchini Guinea na kutengwa kabisa kwa sauti zote zinazoikosoa serikali.” “Kilicho muhimu zaidi kuhusu uamuzi huu ni kwamba kwa kuwazuia wadau wa kisiasa kutenda kisheria na waziwazi, wanalazimishwa kufanya mambo kisiri, huku hatari zote zinazotokana na hili kwa utulivu wa nchi na demokrasia.”

“Tutaendelea kupanga na kupinga utawala huu wa kijeshi kwa sababu kila kitu kinachofanywa leo kinachangia kutokuwa na utulivu wa kisiasa na kijamii wa taifa letu, na hili ni jambo la kusikitisha, kutokana na juhudi zote zilizofanywa ili kuhakikisha kwamba Guinea inatajwa kama mfano miongoni mwa nchi zilizo bora katika suala la demokrasia, uhuru, na hasa uendelezaji wa haki za binadamu.”

Serikali bado haijazungumza chochote.

“Hali mbaya zaidi”

Mashirika ya kiraia pia yamezngumzia kuhusu kuvunjwa kwa vyama 40 vya siasa na Serikali. Kwa upande wa National Front for the Defense of the Constitution (FNDC), uamuzi huu, uliofanywa na sheria ya waziri, unaiingiza nchi katika hali ya kutokuwa na uhakika zaidi.

“Sasa, utawala wa kijeshi bila shaka unaelekea katika utekelezaji wa mfumo wa chama kimoja, ambao kwa bahati mbaya unatukumbusha historia mbaya ya Guinea katika miaka ya 1960. Hali hii imeongezwa tu kwenye orodha ndefu ya ukandamizaji wa uhuru wa umma, ikiwa ni pamoja na watu kutoweka kwa lazima, utekaji nyara, na kufungwa kwa viongozi wa kisiasa na kijamii, miongoni mwa mengine. Kwa hivyo, bila shaka nchi inatumbia katika hali ya kutokuwa na uhakika. Hii ni mbaya zaidi”, amesema Ibrahima Diallo, kiongozi wa National Front for the Defense of the Constitution ndani ya muungano wa upinzani wa Forces Vives

Kwa Rafiou Sow, kiongozi wa Chama cha Urejesho na Maendeleo (PRP) kilichovunjika sasa, “ni dhuluma safi na rahisi.” “Ni sheria ya wenye nguvu zaidi.” “Leo, maadili ya kidemokrasia yametoweka nchini mwetu,” ametangaza. “Waliapa kubadilisha tabaka la kisiasa, na leo hii ndiyo njia yao ya kuchukua hatua. Tulitarajia uamuzi huu. Hatuna sehemu ya kukimbilia, iwe ndani ya mfumo wa haki wa Guinea wala mahali pengine popote.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *