Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ameeleza dhamira ya Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha watanzania hususan vijana, wanapata makazi bora na ya gharama nafuu kupitia miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Majengo (TBA).

Ulega ameyasema hayo jijini Dar es Salaam mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakati ilipotembelea na kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi ya watumishi wa umma katika eneo la Magomeni Kota Awamu ya Pili pamoja na nyumba za makazi za Canadian Village zilizopo Masaki.

Amebainisha kuwa hadi sasa jumla ya nyumba 174 zinaendelea kujengwa katika eneo la Temeke jijini Dar es Salaam kwa lengo la kusaidia vijana kupata makazi ya gharama nafuu na hivyo kupunguza changamoto ya uhaba wa nyumba katika jiji hilo.

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *