Shambulio dhidi ya hospitali nchini Sudan limesababisha vifo vya watu wasiopungua 64, wakiwemo watoto 13, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ameripoti siku ya Jumamosi, akitoa wito wa “ulinzi uliohakikishwa kwa raia, wafanyakazi wa afya, na watoa huduma za kibinadamu.”

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Wakati huu, hospitali ya chuo kikuu katika mji mkuu wa East Darfur, El-Daein, imeshambuliwa na watu wasiopungua 64, wakiwemo watoto 13, manesi wawili, daktari mmoja na wagonjwa kadhaa wameuawa katika shambulio hilo,” Tedros Adhanom Ghebreyesus ameelezea masikitiko yake kwenye mtandao wa kijamii wa X.

Kulingana na WHO, shambulio hilo lilihusisha “silaha nzito” na kulenga kituo cha pili cha afya, pia kuharibu vifaa na akiba.

Vita visivyo isha kati ya washirika wa zamani tangu mwaka 2023, vimeongezeka katika miezi ya hivi karibuni huku kukiwa na ongezeko la mashambulizi mabaya ya ndege zisizo na rubani katika maeneo ya makazi yenye watu wengi, shule, na hospitali.

Eneo kubwa la magharibi mwa Darfur sasa linadhibitiwa kwa kiasi kikubwa na wanamgambo wa RSF, huku jeshi likidhibiti mashariki, katikati, na kaskazini mwa Sudan.

“Damu ya kutosha imemwagika. Mateso ya kutosha yamesababishwa. Ni wakati wa kupunguza mzozo nchini Sudan na kuhakikisha ulinzi wa raia, wafanyakazi wa matibabu, na watoa misaada ya kibinadamu,” ameomba Tedros Adhanom Ghebreyesus.

Ofisi ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan ilisema Jumamosi kwamba “ilishangazwa na shambulio dhidi ya hospitali huko Mashariki mwa Darfur siku ya Ijumaa, ambalo linaripotiwa kuua watu kadhaa, wakiwemo watoto, na kujeruhi wengine wengi.”

Jiji linalodhibitiwa na wanamgambo

Shirika lisilo la kiserikali la Emergency Lawyers, kundi huru linaloandika kuhusu mzozo wa Sudan kati ya jeshi na Vkosi vya Msaada wa Haraka (RSF), liliripoti kwamba shambulio hilo lililenga Hospitali ya Chuo Kikuu cha El-Daein.

El-Daein, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Mashariki, ambalo linadhibitiwa na RSF, hulengwa mara kwa mara na jeshi, ambalo linajaribu kuwaondoa wanamgamo wa eneo hilo kutoka kwenye ukanda wa kati wa Sudan.

Katika taarifa iliyonukuliwa na shirika la habari laserikali la SUNA, jeshi la Sudan limebainisha kwamba “linaheshimu kanuni na sheria za kimataifa” na, bila kuishutumu moja kwa moja RSF kwa kushambulia hospitali, limebainisha kwamba aina hii ya kitendo ni “kitendo kinachoendelea na shughuli ya kila siku” ya wanajeshi wa eneo hilo.

Shambulio la mwezi Machi, kwenye soko la El-Daein, lilisababisha mapipa ya mafutankuungua kwa saa nyingi.

Licha ya kulaaniwa mara kwa mara kutoka kwa Umoja wa Mataifa, hospitali zinaendelea kulengwa.

Karibu miaka mitatu ya vita nchini Sudan imewaua makumi ya maelfu ya watu na kusababisha zaidi ya milioni 11 kuhama makazi yao, na kusababisha kile ambacho Umoja wa Mataifa unakiita mgogoro mbaya zaidi wa kibinadamu duniani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *