.

Chanzo cha picha, Getty Images

Mwigizaji na msanii wa mapigano ya judo, Chuck
Norris alifariki dunia jana asubuhi akiwa na umri wa miaka 86, familia yake
imetangaza kupitia mtandao wa Instagram.

Norris
alilazwa hospitalini huko Hawaii kabla ya kifo chake

Norris
alilazwa hospitalini huko Hawaii kwa dharura ya kimatibabu kabla ya kifo chake,
TMZ iliripoti hapo awali.

Katika
taarifa yao, familia yake ilisema wanapendelea kuweka hali hiyo kuwa ya siri,
lakini walielezea kifo cha Norris kama kilichotokea “ghafla”.

‘Hamkuwa
mashabiki tu, mlikuwa marafiki zake’ – taarifa kamili ya familia

Tunasikitika
kama familia kutangaza kifo cha ghafla cha mpendwa wetu Chuck Norris
kilichotokea jana asubuhi. Ingawa tungependa kuweka hali hiyo kuwa ya faragha,
tafadhali jua kwamba alikuwa amezungukwa na familia yake na alituacha akiwa na
amani.

“Kwa ulimwengu, alikuwa msanii wa mapigano ya judo,
mwigizaji, na nembo ya nguvu. Kwetu, alikuwa mume aliyejitolea, baba na babu mwenye
upendo, ndugu wa kipekee, na kitovu cha familia”

Aliishi
maisha yake kwa imani, kusudi, na kujitolea bila kuyumba kwa watu aliowapenda.
Kupitia kazi yake, nidhamu, na wema wake, alitoa hamasa kwa mamilioni duniani
kote na mchango wake utakumbukwa na wengi daima.

Ingawa
mioyo yetu imeumia, tunashukuru sana kwa maisha aliyoishi na kwa nyakati
zisizosahaulika tulizobarikiwa kushirikishana naye. Upendo na uungwaji mkono
aliopata kutoka kwa mashabiki kote ulimwenguni ulikuwa na maana kubwa kwake, na
familia yetu inawashukuru sana kwa hilo. Kwake, hamkuwa mashabiki tu, mlikuwa
marafiki zake.

Tunajua
wengi wenu mmesikia kuhusu kulazwa kwake hospitalini hivi karibuni, na
tunashukuru sana kwa maombi na usaidizi mliompa.

Tunapoomboleza
msiba huu, tunaomba faragha kwa ajili ya familia yetu wakati huu. Asante kwa
kumpenda pamoja nasi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *