Mwanamke wa Kiambu Aliyechomewa Gari Wakati wa Maandamano Githurai AzungumzaMwanamke wa Kiambu Aliyechomewa Gari Wakati wa Maandamano Githurai Azungumza

Mwanamke mmoja wa Kiambu pamoja na mumewe sasa wanahesabu hasara baada ya gari lao kuchomwa moto na waandamanaji huko Githurai mapema leo, Jumatatu, Mei 18.

Priscilla
Priscilla alisema waandamanaji waliona skafu yenye chapa ya UDA kwenye gari lake.
Source: Facebook

Jumatatu, shughuli za usafiri nchini zilisimama kutokana na maandamano yaliyosababishwa na ongezeko la kihistoria la bei ya mafuta nchini, kama ilivyotangazwa hivi karibuni na Mamlaka ya Kudhibiti Nishati na Petroli (EPRA).

Priscillah anasimulia jinsi gari lake lilivyochomwa huko Githurai

Huko Githurai, gari jeusi lilichomwa moto na waandamanaji, na mmiliki wake sasa anasimulia jinsi kuwa na vifaa vya kampeni vya UDA ndani ya gari hilo kulivyosababisha tukio hilo.

Akizungumza na wanahabari, Priscilla alisimulia kwamba mumewe ndiye alikuwa akiendesha gari hilo alipokutana na waandamanaji hao wenye vurugu.

“Mume wangu alikuwa huru, kwa hiyo nikamwomba aendeshe hadi Kamakis kununua vifaa vya ujenzi huko Kamakis. Hatukujua kwamba maandamano yangekuwa ya vurugu kiasi hiki kwa sababu yalikuwa yameelezewa kama maandamano ya amani. Hata hivyo, alipofika Githurai, mambo yaliharibika baada ya waandamanaji kuona baadhi ya vifaa vya kampeni vya UDA ndani ya gari,” alisema.

Pia soma

Magazetini Wahudumu wa Matatu Watangaza Kusitisha Shughuli Kufuatia Gharama ya Mafuta

Kulingana na Priscilla, waandamanaji walichoma gari hilo moto huku mumewe akinusurika kwa shida na kujiokoa.

“Walikasirishwa na vifaa vya kampeni vya UDA, ambavyo ni vyangu kwa sababu ninagombea kiti cha MCA katika uchaguzi ujao. Walianza kwa kuvunja madirisha kabla ya kuchoma gari hilo moto,” aliongeza.

Gari hilo lililopatwa na mkasa lilikuwa Mazda CX 5 nyeusi.

Mwanamke huyo alisema mumewe aliripoti suala hilo katika Kituo cha Polisi cha Kasarani, akiongeza kuwa bado hawajapata ujasiri wa kwenda kuangalia kilichobaki cha gari lao.

“Tunahope kwenda kesho kuona kama kuna chochote kinachoweza kuokolewa,” alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *