
Tangu Mei 22, Shirika la Afya Duniani (WHO) limeongeza hatari inayosababishwa na mlipuko wa virusi vya Ebola kwa afya ya umma mashariki mwa DRC kwa kiwangu cha “juu sana.” Ingawa hatari katika ngazi za kikanda na kimataifa hazijabadilika, mkurugenzi wake, Tedros Adhanom Ghebreyesus, anaamini janga hili linaenea kwa kasi. Mwitikio unaendelea, haswa katika mkoa wa Ituri, jimbo lililoathiriwa zaidi. Lakini ili kupambana na ugonjwa huo, mwitikio hauwezi kuwa wa kimatibabu pekee.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Kinshasa, Paulina Zidi
Wote wanaofanya kazi katika maeneo yaliyoathirika wanasisitiza hoja hii: ni muhimu kujenga uhusiano wa uaminifu na wakazi wa maeneo yaliyoathiriwa. Na Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka wamebainisha katika taarifa kwa vyombo vya habari: “Mfumo mzima wa mwitikio hauwezi kufanya kazi bila ushiriki endelevu wa jamii.”
Hili ni kweli hasa katika mkao ulio na vurugu na ukosefu wa usalama. Msimamo ulioshirikiwa na Frederica Badocco, mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Solidarité Internationale nchini DRC, ambaye anasema “ushiriki wa jamii ni muhimu sana kwa kutekeleza shughuli na kuwezesha timu kufanya shughuli hizi kwa usalama.”
Hii ndiyo maana sasa ni muhimu kwa wafanyakazi wa kibinadamu kushirikiana na viongozi wa jamii na jamii mashariki mwa DRC “kabla ya kupeleka timu, ili kuongeza uelewa miongoni mwa watu kuhusu suala hilo,” anabainisha mkuu wa ujumbe huo.
“Uelewa huu wa jamii bado hautoshi,” anaonya mfanyakazi wa kibinadamu aliyepo Mongwalu, kitovu cha mlipuko huo. Kampeni za uhamasishaji kwa wingi kupitia redio au mabango zinafanya kazi vizuri, lakini pia kuna haja ya kuwafikia watu wa kawaida, kwa mfano, kupitia ziara za nyumba kwa nyumba. “Na hapo ndipo tumechelewa nyuma,” anaongeza mfanyakazi huyu wa kibinadamu.
