Senegal: Ousmane Sonko achaguliwa kuwa Spika wa BungeSenegal: Ousmane Sonko achaguliwa kuwa Spika wa Bunge

Nchini Senegal, aliyekuwa waziri mkuu wa Senegal Ousmane Sonko, ambaye alifutwa kazi Mei 22, amechaguliwa kuwa Sika wa Bunge Mei 26, 2026, huko Dakar, kwa kura 132 kati ya kura 133 zilizopigwa. Uchaguzi umefanyika bila ya wanachama thelathini wa upinzani waliopinga uhalali wa kurejeshwa kwake kama mbunge. Anamrithi Malick Ndiaye, aliyejiuzulu Mei 24, na anachukua majukumu yake mara moja.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Dakar, Léa-Lisa Westerhoff

Hii inaashiria hatua mpya katika mabadiliko katika ngazi za juu za serikali, kufuatia uteuzi wa Ahmadou Al Aminou Mohamed Lô kama kiongozi wa serikali Mei 25.

Kwa hivyo, Waziri mkuu wa zamani anakuwa kiongozi wa pili muhimu zaidi nchini Senegal, baada ya kuchaguliwa kama Spika wa Bunge, huku wabunge kutoka chama cha PASTEF wakikaribisha kwa makofi mengi, wengi wao wakiwa wamevaa nguo nyeupe kwa ajili ya hafla hiyo.

Ousmane Sonko amezungumza kwa kirefu, akikaribisha uteuzi wa kiongozi mpya wa serikali siku iliyotangulia, Ahmadou Al Aminou Mohamed Lô, ambaye alimtaja kama mtu mwaminifu na mchapakazi. Sonko pia amesema kwamba chama chake hakikuhusika katika uteuzi huo au mashauriano kuhusu serikali mpya.

Licha ya mwanzo huu mgumu, Ousmane Sonko amesema kwamba PASTEF bado yuko wazi “kwa majadiliano yenye uwajibikaji ambayo huweka kando ubinafsi ili kumaliza muhula huu kwa njia bora zaidi”: “PASTEF, ambayo ni chama cha siasa—na hii haijawahi kutokea katika historia ya kisiasa ya nchi hii na labda duniani—ambapo wengi katika upinzani na serikalini, bado wako wazi kwa majadiliano yenye uwajibikaji ambayo huweka kando ubinafsi ili kutafuta njia bora na uwezo kwa ajili ya utawala wa amani na kumaliza muhula huu katika mazingira bora,” Ousmane Sonko ametangaza leo Jumanne huko Dakar, baada ya kuchaguliwa kwake.

“Hatuwezi kuwa katika mfumo wa utendaji unaompa rais mamlaka makubwa kupita kiasi”

“Na majadiliano haya hayatajadili kuhusu wanaume na wanawake.” Yatazunguka miongozo na programu, ambayo sasa lazima tukubaliane na Rais wa Jamhuri, ili kuzingatia kuendelea kumuunga mkono kwa utulivu. “Hatuwezi kuwa na mfumo wa utendaji unaompa Rais mamlaka makubwa kupita kiasi nchini Senegal leo,” ameongeza.

Kwa hivyo, huu ni ujumbe unaondoa hofu, licha ya maneno machache yaliyoelekezwa kwa Rais Bassirou Diomaye Faye.

Bado haijabainika kama Senegal itapata njia ya kurudi kwenye utendaji kazi wa amani zaidi wa taasisi zake. Kwa sababu uchaguzi wa Ousmane Sonko unapingwa kwa misingi ya kisheria: Wabunge 32 wa upinzani kati ya 165 wanaounda Bunge la itaifa walitoka nje ya bunge kwa kelele wakati wa uchaguzi wa Spika mpya, wakikataa uhalali wa kurejeshwa kwa Sonko kama mbunge, ikizingatiwa kwamba hapo awali alikuwa Waziri Mkuu na kwa hivyo alikuwa amepoteza mamlaka yake ya kuchaguliwa, ambayo alikuwa ameshinda katika uchaguzi wa wabunge wa mwezi Novemba 2024.

Lakini, bila kushangaza, katika bunge lililotawaliwa na chama tawala cha PASTEF, kura iliendelea. Kwa Marie Rose Faye, msemaji wa African Patriots of Senegal for Work, Ethics, and Fraternity (PASTEF), mara tu ofisi ya kisiasa ya Bunge ilipothibitisha uhalali wa kurejeshwa kwa Sonko kama mbunge, utaratibu huo ulikuwa “halali kabisa.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *