tuna

Chanzo cha picha, x

    • Author, Yusuph Mazimu
    • Nafasi,

Kwa siku kadhaa sasa kuna sauti mbili zinazoshindana katika mdundo wa ngoma mbili tofauti lakini kwenye uwanja mmoja. Sauti moja inasema No Reform No Election, ikisisitiza mageuzi ya msingi kwanza kufanyika kabla ya uchaguzi. Sauti nyingine ikiitika; Oktoba Tunatiki, kauli ya ujasiri wa kusonga mbele, hata bila dhamana ya mabadiliko kamili.

Huu si ubishi wa kawaida. Ni mgongano wa falsafa, mtazamo na matarajio. Ni sauti ya kizazi kipya kinachotafuta nafasi ya kusema, kuamua, na kudai hata kama ni kwa kupitia ujumbe wenye maneno mawili au matano.

Katika nchi ambayo historia ya uchaguzi wake imejaa mchanganyiko wa changamoto na matumaini kutokana na uchanga wake kwenye demokrasia, sasa tunashuhudia aina mpya ya siasa na harakati. Siana na harakati zisizo na silaha, bali hashtags, ujumbe, picha, sauti na video. Harakati zisizo na maandamano wala matusi, bali machapisho mitandaoni.

Lakini je, huu mgongano huu unaisha kwenye mitandao au unatafsiriwa katika uhalisia wa siasa ya Tanzania?



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *