
Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif amesema kuwa makubaliano kati ya Iran na Marekani kwa lengo la kukumaliza vita yapo “karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote,” huku yakitarajiwa kukamilika ndani ya saa 24 zijazo.
Sharif, ambaye nchi yake imekuwa mpatanishi wa mazungumzo kati ya Iran na Marekani, aliandika katika akaunti yake ya X siku ya Jumamosi kwamba hafla ya utiaji saini wa kielektroniki itafuata mara baada ya kukamilika.
Ameongeza kuwa mazungumzo ya ngazi ya kiufundi yamepangwa kufanyika wiki ijayo baada ya kusainiwa makubaliano ya kielektroniki.
“Tunakaribia kufikia makubaliano ya amani kuwahi kufikiwa kuliko hapo awali. Makubaliano haya yanatazamia kukamilika muda wa saa 24 zijazo; Pakistan inajiandaa kwa ajili ya kutia saini mkataba wa amani wa kielektroniki mara tu baada ya hapo, utakaofuatiwa na mazungumzo ya ngazi ya kiufundi wiki ijayo,” ameandika Waziri Mkuu wa Pakistan katika akaunti yake ya X.
Akizungumza katika mahojiano ya televisheni siku ya Ijumaa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi alisema juhudi za kidiplomasia zenye lengo la kuthibitisha ushindi wa Jamhuri ya Kiislamu katika vita vya kichokozi vya Marekani na Israel sasa ziko katika hatua za mwisho kwa kuzingatia hati ya maelewano yenye vipengele 14 ambayo imejadiliwa katika vyombo vya habari.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baghaei jana alisema kuwa Tehran inasalia na mashaka kuhusu diplomasia na Marekani kutokana na rekodi ya Washington ya kukiuka ahadi zake, na kuongeza kuwa hakuna safari yoyote ya kwenda Geneva iliyopangwa katika muda wa siku mbili zijazo huku kukiwa na ripoti za uwezekano wa makubaliano na Marekani.