
Baada ya kusubiri kwa siku kadhaa na uvumi kuendeea, ndege ya kwanza iliyobeba wahamiaji waliofukuzwa nchini Marekani imetua katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui, siku ya Ijumaa jioni, Juni 12.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Operesheni hiyo ilifanywa kwa siri, na maelezo yake bado hayajaeleweka. Mamlaka haijazungumza chochote kuhusu uhamisho kuwasili kwa raia hao. Kuwasili huku ni sehemu ya mkakati wa utawala wa Marekani wa kuwahamisha baadhi ya wahamiaji kwenda nchi za ulimwengu wa tatu. Jamhuri ya Afrika ya Kati ndiyo nchi ya hivi karibuni ya Afrika kukubali mpango kama huo.
Safari ya saa 24. Ikiondoka Alexandria, Louisiana, ndege hiyo ilisimama kwa mara ya kwanza Accra kabla ya kutua Bangui yapata saa 4:00 usiku. Kikosi kikubwa cha maafisa wa polisi kilitumwa kwa siri kubwa kusimamia kuwasili kwa wahamiaji hao kutoka Marekani.
Kulingana na chanzo cha uwanja wa ndege, wahamiaji hao – wanaoripotiwa kuwa 17 kwa idadi – walitumia karibu saa nne katika kituo cha polisi cha uwanja wa ndege wakikamilisha taratibu za kiutawala.
Wakiwa wamesindikizwa katikati ya usiku, watu hawa kwa sasa wanapewa hifadhi katika hoteli mbili katikati mwa jiji la mji mkuu.
Hakika, hakuna taarifa kuhusu uraia wao, hadhi yao, au hali ya mapokezi yao nchini. Hali hii imeibua maswali miongoni mwa mashirika ya kiraia, ambayo yanalaani ukosefu wa uwazi na yana wasiwasi kuhusu mustakabali wa wahamiaji hao.
Msemaji wa kikundi kazi cha mashirika ya kiraia, Paul-Crescent Beninga, alisema: “Licha ya maombi yetu mengi ya ufafanuzi, serikali imechagua ukimya na dharau.” “
Upinzani wa kisiasa, kwa upande wake, unasema umekatishwa tamaa na kushtuka. Unashuku serikali kupokea kiasi kikubwa cha pesa kama sehemu ya operesheni hii na kwa hivyo unahitaji maelezo kuhusu masharti ya makubaliano haya na Marekani.