A

Chanzo cha picha, ACT

Hatma ya mgombea urais kupitia ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina, ipo njia panda baada ya Msajili wa Vyama vya Siasa kutangaza kuwa uteuzi wake haujakidhi matakwa ya kikanuni, kufuatia pingamizi lililowasilishwa na mwanachama wa chama hicho, Monalisa Ndala.

Katika uamuzi uliotolewa leo, Msajili alibainisha kuwa Mpina hakutimiza vigezo vya uanachama kwa mujibu wa kanuni za chama, akisema kuwa alijiunga ACT-Wazalendo nje ya muda uliopangwa na hivyo hakustahili kuwania nafasi ya urais kupitia chama hicho.

Hata hivyo, uongozi wa ACT-Wazalendo kupitia Katibu Mkuu, Ado Shaibu, umetangaza kutopokea uamuzi huo na kueleza kuwa tayari wameanza mchakato wa kufungua kesi Mahakama Kuu ili kupinga hatua ya Msajili, wakidai imekiuka taratibu na kuingilia mchakato wa ndani wa chama.

“Chama cha ACT Wazalendo kinaweka msimamo kuwa hakitofuata maelekezo ya Msajili wa Vyama vya siasa juu ya suala hili” inasema taarifa ya ACT na kuongeza kuwa katika kesi itakayofungua itaweka zuio dhidi ya utekelezaji wa uamuzi huu hadi kesi ya msingiisikilizwe.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *