- Mume wa marehemu mwimbaji wa nyimbo za injili Betty Bayo ameonekana kana kwamba hajaguswa kabisa katika video ya TikTok iliyosambaa mitandaoni, licha ya drama kubwa inayoendelea kuhusisha familia yake
- Mjadala huo mtandaoni ulianza kutokana na tuhuma nzito zilizotolewa na rafiki mkubwa wa Bayo pamoja na baba mzazi wa watoto hao, Mchungaji Victor Kanyari, ambao wote wanadai kuwa Tash hawasimamii watoto hao ipasavyo
- Licha ya malalamiko ya Kanyari hadharani akitaka watoto wake warejeshwe kwake, binti wa Bayo, Sky, hivi karibuni alimtetea vikali baba yake wa kambo
Video ya mjane wa Betty Bayo, Hiram Gitau maarufu kama Tash, imekuwa ikisambaa mtandaoni ikionyesha jinsi ambavyo hajali kelele zinazoendelea kumzunguka yeye na familia yake.

Source: TikTok
Yote yalianza baada ya rafiki mkubwa wa Bayo, Shiro Stuart, kujitokeza na kutoa tuhuma dhidi ya Tash, akidai kwamba alikuwa akiwatendea watoto vibaya na pia akihifadhi fedha ambazo Sky alikuwa akipata kama mshawishi wa mitandao ya kijamii.
Muda mfupi baadaye, binti wa Bayo, Sky, alijitokeza na kumtetea Tash kwa nguvu. Alikanusha madai kwamba Tash anachukua au kuhifadhi fedha zake na akasisitiza kuwa hakuna mtu anayemlazimisha kusema chochote wala hamdanganyi au kumtumia kwa manufaa yao.
Hata hivyo, wakati wa ibada ya Jumapili kanisani kwake, baba mzazi wa Sky, Mchungaji Victor Kanyari, alimshambulia vikali Tash kwa maneno, akimshutumu kwa kuwatumia watoto wake kujinufaisha kifedha.
Je, Tash alijibu tuhuma zinazoendelea dhidi yake?
Kanyari pia alidai kuwa watoto wake walikuwa wamekaa nyumbani kwa wiki kadhaa na kwamba ilibidi Naibu Rais Kithure Kindiki aingilie kati na kulipa ada ya shule ya watoto hao.
Aidha, Kanyari alihoji kwa nini Tash hataki kuwa pamoja na watoto wake wa kumzaa na badala yake awarudishe Sky na Danny kwake.
Katikati ya tuhuma zinazoendelea kutoka kwa watu waliokuwa karibu na Betty Bayo, Tash ameendelea kudumisha ukimya wake.
Rafiki yake, anayejulikana kwenye TikTok kwa jina la @Frankmash, alishiriki video ya kuchekesha ambayo ilionekana kama jibu lisilo la moja kwa moja kwa kelele na mijadala inayoendelea kumhusu.
Katika video hiyo, Tash alikuwa amevaa fulana nyeusi na kaptura nyekundu huku akiwa ameketi nje ya kibandaski kinachoonekana kuuza chakula, wakifurahia mlo wao.
Wakati mmoja, alionyesha kilichokuwa kwenye sahani yake — githeri iliyopikwa vizuri — huku akicheka na kuonekana kufurahia wakati huo.
Rafiki huyo pia alichagua sauti ya video iliyokuwa na mtu anayelalamika na kupiga kelele kiasi kwamba maneno yake yalionekana kama porojo zisizoeleweka.
Hadi sasa, Tash hajawahi kujibu hadharani tuhuma zozote zilizotolewa dhidi yake tangu mke wake alipofariki dunia.
Tazama video hapa chini:
Haya ni baadhi ya maoni ya watumiaji wa mitandao ya kijamii:
@Janet Katile alisema: “Tash hajibu kelele.”
@Essie alisema: “Mimi siwezi chukia Tash juu ya maneno ya watu. I love him.”
@Caroh Maina alisema: “Huyu hukuwa nani kwa Tash? Yeye huwa anamuunga mkono kila wakati.”
@Winnie alisema: “Huyu naye huwa hajali kabisa.”
@Only Child alisema: “Mungu, tafadhali, nahitaji Tash katika maisha yangu.”
@Abuh alisema: “Napenda utulivu wake katikati ya makelele na hasira zote.”
@Essy alisema: “Mungu wa Betty Bayo atasimama na wewe, nyamaza tu hata usiongee.”

Source: TikTok
Tash alimwambia nini Sky?
Kwingineko, video iliyosambaa hivi karibuni ilimuonyesha Tash akikatiza matangazo ya moja kwa moja ya TikTok ya binti yake wa kambo, Sky, ili kumkumbusha kuhusu usiku wa familia wa kutazama filamu waliokuwa wameupanga.
Tukio hilo lilitokea wakati kulikuwa na tuhuma za umma kutoka kwa rafiki wa karibu wa Betty Bayo aliyedai kuwa Tash alikuwa akimfundisha Sky nini cha kusema kila mara madai mapya yanapoibuka dhidi yake.

Pia soma
Lakewood Premier School: Mwanafunzi wa Gredi ya 9 afariki shuleni, alidondoka kutoka ghorofa ya 3
Wakati wa matangazo hayo ya moja kwa moja, Sky pia aliisifia nywele za baba yake wa kambo kabla ya kumwambia kwamba angejiunga nao muda mfupi baadaye.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke

