Chanzo cha picha, Getty Images
Axios imeripoti kuwa Tehran na Washington zimekubaliana kusitisha mashambulizi katika Ghuba ya Uajemi na kufanya mazungumzo ya moja kwa moja katika siku chache zijazo mjini Doha, Qatar.
Mwandishi wa Axios, Barak Ravid, aliandika Jumapili jioni kwamba afisa mmoja mwandamizi wa Marekani amesema Marekani na Iran zimekubaliana kuacha kushambuliana, na kwamba pande hizo mbili zinatarajiwa kukutana mjini Doha siku ya Jumanne kutafuta suluhu ya tofauti zao kuhusu Mlango wa Hormuz.
Kwa mujibu wa Axios, mazungumzo hayo yataangazia zaidi suala la Mlango wa Hormuz.
Iran imehusisha mapigano mapya na Marekani na kile inachodai kuwa ni kuingilia usimamizi wake wa Mlango wa Hormuz.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema wakati wa ziara yake nchini Iraq kwamba kufunguliwa kikamilifu kwa Mlango wa Hormuz, kwa mujibu wa makubaliano na Marekani, ni jukumu la Tehran pekee, na kwamba kuingilia mchakato huo kutavuruga juhudi hizo na kuongeza mvutano katika eneo hilo.
Maelezo zaidi: