Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa jukumu la kupanga na kusimamia shughuli katika Mlango-Bahari wa Hormuz ni la Iran pekee, akisisitiza kwamba hakuna taasisi wala nchi nyingine yenye mamlaka au wajibu katika suala hilo.

Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, amesema kuwa kwa mujibu wa hati ya makubaliano (MoU), Mlango-Bahari wa Hormuz utarejea katika hali yake ya kawaida ya kufanya kazi ndani ya siku 30, chini ya usimamizi utakaowekwa na Iran.

Akizungumza katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari jijini Baghdad pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fuad Hussein, Araghchi alisema serikali ya Iraq iliunga mkono wananchi wa Iran kama waathiriwa wa shambulio hilo.

Aidha, alisema wananchi wa Iraq walionesha mshikamano mkubwa na kutoa uungwaji mkono kwa watu wa Iran, jambo ambalo, kwa mujibu wake, liliwatia moyo na kuwapa faraja wananchi wa Iran katika kipindi hicho.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kwa mujibu wa kifungu cha kwanza cha hati ya makubaliano (Memorandum of Understanding), vita vinapaswa kukomeshwa katika maeneo yote, ikiwemo Lebanon.

Araghchi alisema Iran inasikitishwa na kuendelea kwa mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon, akisisitiza kuwa hali hiyo inakiuka makubaliano yaliyofikiwa.

Aliongeza kuwa Marekani ina wajibu wa kutekeleza ahadi iliyoichukua kwa niaba yake na Israel katika hati hiyo ya makubaliano, kwa kuhakikisha mashambulizi hayo yanakoma na kuwezesha utekelezaji wa usitishaji vita nchini Lebanon.

 

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *