• Mary Claire Ochieng amefichua kuwa aliyekuwa mpenzi wake alipanga shambulio la kutisha la tindikali baada ya wao kuachana, na kwa sasa anaendelea kupokea matibabu hospitalini
  • Alishiriki jumbe za vitisho kutoka kwa Elvis, ambaye alidai kuwa alimwelezea mapenzi yake lakini pia akasema “kifo pekee ndicho kingewatenganisha,” na alipokataa kurudiana naye, alidaiwa kupanga shambulio la tindikali
  • Wakenya wameonyesha huruma, tahadhari na kuanzisha mjadala kuhusu mapenzi na uwekezaji katika mahusiano kufuatia simulizi ya kusikitisha ya Claire na Elvis

Nairobi, Kenya: Mary Claire Ochieng, mwanamke aliyeshambuliwa kikatili kwa tindikali, amesema kuwa aliyekuwa mpenzi wake, Elvis, hakuwahi kumlipia ada ya shule wakati wowote.

Mwimbaji wa SDA Aliyeshambuliwa kwa Tindikali Azungumzia Madai Ex Wake Alimlipia Kari ya Shule
Mwimbaji wa SDA Aliyeshambuliwa kwa Tindikali Azungumzia Madai Ex Wake Alimlipia Kari ya Shule
Source: Facebook

Claire hivi karibuni alizungumza hadharani kwa mara ya kwanza tangu kushambuliwa katika tukio hilo la kutisha, na akasimulia jinsi mambo yalivyoanza kuharibika hata kabla ya Machi 2026.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 25, aliyekuwa mpenzi wake alipanga shambulio hilo baada ya yeye kuvunja uhusiano wao alipogundua kuwa alikuwa ameoa na alikuwa na watoto wawili.

Pia soma

Miezi 3 Baada ya Shambulio la Tindikali, Mary Claire Afunguka na Kufichua Ujumbe wa Kutisha

Claire alishiriki jumbe za kutisha za WhatsApp ambazo mshukiwa alidaiwa kumtumia akimwelezea mapenzi yake huku pia akimtishia kwamba “kifo pekee ndicho kingewatenganisha.”

Nani alilipia masomo ya Claire chuoni?

Kwa mujibu wa mwimbaji huyo wa nyimbo za injili, kulikuwa na mashambulizi saba yaliyodaiwa kufanywa dhidi yake, matatu kati yake yakihusisha tindikali.

Wawili hao walikutana mwaka 2019, na wakaanza uhusiano wa kimapenzi miaka mitatu baadaye.

Huduma ya kutafuta habari sasa inapatikana TUKO! Tafuta kwa urahisi mada au watu unaopenda kusoma kuwahusu kupitia sehemu ya juu kulia ya ukurasa.

Wakati nilipokutana naye nilikuwa tayari nipo chuoni. Nilikuwa mwanafunzi aliyedhaminiwa na serikali, na familia yangu iliweza kugharamia gharama zilizobaki katika kipindi chote cha miaka minne ya masomo yangu,” alisema.

“Mwezi Aprili niliamua kuondoka kabisa kwenye uhusiano huo, na kufikia Januari 2026 nilikuwa nimeuvunja kabisa,” alisema.

Wakenya walivyoitikia simulizi hiyo

Apondi Vee:

“Claire, hii ni simulizi yako. Mungu akupe uponaji wa haraka. Nimependa ulivyomwambia kwamba ungependa kufa kuliko kutoka kimapenzi kwa sababu ya pesa. Hivyo ndivyo nilivyoona kwenye jumbe. Mungu akufariji. Simulia simulizi yako bila woga, kwa sababu ukifanya hivyo hakuna mtu atakayeitumia dhidi yako.”

Pia soma

“Nilimsubiri Wakati wa Mungu”: Mwanamke Atunza Ubikra Wake na Kuolewa Akiwa na Miaka 69

Monik Albert:

“Nimeona miamala hiyo ni ya kweli. Alikataa iPhone 17, akaishia kumwagiwa tindikali. Tafadhali mwachilieni huyo jamaa mniletee mimi nitamrekebisha.”

Philip Kariuki:

“Hadithi hii yote inahusu mapenzi. Usifanye ujinga wa kumuumiza mtoto wa mtu kwa sababu amesema hakutaki. Endelea na maisha yako. Wanawake ni wengi sana, lakini muhimu zaidi usiwekeze kwa mtu kwa matarajio makubwa, maana mwisho unaweza kuumia.”

Macj Jimes:

“Chukulia mapenzi kama kamari. Ukiwekeza ukapoteza, songa mbele. Ukishinda, hiyo ndiyo bahati yako. Hakuna sababu yoyote inayoweza kuhalalisha jambo hili. Mimi huwa ninawaombea hata wapenzi wangu wa zamani waishi waone jinsi ninavyofurahia maisha ambayo walidhani singeyafikia. Nawashukuru wote walioniacha kwa sababu walinipa motisha ya kufanya kazi kwa bidii na kujiboresha.”

Bwire Ke:

“Ni vizuri kwamba ametoa upande wake wa hadithi. Sasa wanaomhukumu wanaweza kupumzika.”

Leaa Gashumba:

“Nimeona hapo M-Pesa ya KSh 200,000. Mimi mtu akinitumia hata KSh 10,000 tu naolewa. Sitaki kujua kama ameoa; shida nilizopitia zinanitosha.”

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *