Moto mkali umeteketeza baa moja huko Bangkok mapema siku ya Jumatatu asubuhi, na kuua watu wasiopungua 27 kabla ya wazima moto kuweza kuudhibiti, mamlaka zimesema.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Na: RFI na mashirika mengine

Matangazo ya kibiashara

Picha zilizorushwa mtandaoni na idara ya huduma za dharura zinaonyesha moto mkali na moshi mwingi ukitoka kwenye mlango wa baa ya Na Ladprao, iliyoko kaskazini mwa Bangkok, Thailand. Watu wanaweza kuonekana wakijaribu kukimbia huku moshi mzito mweusi ukipanda angani.

Idara ya huduma za dharura imesema kwamba moto huo uliripotiwa karibu usiku wa manane, saa za huko. Waziri Mkuu wa Thailand Anutin Charnvirakul amewaambia waandishi wa habari katika eneo la tukio kwamba watu 27 wamefariki na majeruhi kadhaa wamepelekwa hospitalini. Ameongeza kuwa chanzo cha moto huo kinachunguzwa.

Moshi kutoka kwa kivunja mzunguko

Anutin Charnvirakul ameripoti simulizi ya mwanamuziki aliyekuwa akitumbuiza katika kituo hicho: mwanamuziki huyo alieleza kwamba aliona moshi ukitoka kwa kivunja mzunguko karibu na jukwaa kabla tu ya kukatika kwa umeme, ikifuatiwa na mlipuko na kuenea kwa kasi kwa moshi mzito. Waathiriwa wengi walipatikana katika vyoo, vilivyoko nyuma ya baa, Waziri Mkuu alisema.

Iliwachukua wazima moto kama nusu saa kudhibiti moto huo. Picha zilizopigwa baada ya moto zinanyesha meza na viti vilivyoungua, pamoja na vitu vingi ndani ya baa vilivyoharibiwa.

Janga linalojirudia

Thailand imepitia majanga kama hayo hapo awali. Mnamo mwaka 2022, watu 14 walifariki katika kisa cha moto katika baa ya muziki mashariki mwa nchi.

Zaidi ya miaka kumi iliyopita, watu 66 waliangamia na wengine zaidi ya 200 walijeruhiwa katika kisa cha moto uliozuka wakati wa sherehe za Mwaka Mpya mnamo Januari 1, 2009, katika klabu ya usiku ya Santika huko Bangkok. Inaonekana moto huo ulisababishwa na fataki zilizorushwa ndani ya jengo hilo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *