G

Chanzo cha picha, SOCIAL MEDIA

Marekani imeanzisha wimbi la sita la mashambulizi ya anga dhidi ya Iran, yakilenga uwanja wa ndege, kituo cha reli na madaraja kadhaa kusini mwa nchi karibu na Mlango Bahari wa Hormuz, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali ya Iran.

Shirika la habari la Tasnim limeripoti kuwa ndege za kivita za Marekani zilirusha makombora yaliyolenga Uwanja wa Ndege wa Iranshahr, bila kutoa taarifa kuhusu kiwango cha uharibifu au iwapo kulikuwa na majeruhi.

Shirika rasmi la habari la Iran na televisheni ya taifa vilisema milipuko mitatu ilisikika karibu na uwanja huo wa ndege, vikiongeza kuwa angalau kombora moja la Marekani lilipiga uwanja huo.

Wakati huo huo, shirika la habari la Fars liliripoti kuwa daraja katika mji wa Bandar Khamir lililengwa katika shambulio la Marekani.

Tasnim pia lilisema mashambulizi ya Marekani yalilenga madaraja matatu katika eneo la Khamir, mkoani Hormozgan.

Mojawapo ya madaraja hayo linaunganisha Bandar Abbas na mji wa Lar katika mkoa wa Fars.

Kwa mujibu wa Tasnim, mashambulizi hayo yalisababisha kukatika kwa umeme katika baadhi ya maeneo na kuvuruga huduma za mawasiliano ya simu. Marekani haijatoa tamko rasmi kuhusu mashambulizi hayo wala madai yaliyotolewa na vyombo vya habari vya Iran.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *