
Rais wa Burkina Fasio Kapteni Ibrahim Traoré, amehutubia wakazi wa mji wa Yaadga, kaskazini mwa Burkina Faso, siku ya Alhamisi, Julai 16, 2026, katika hotuba ndefu. Alijadili maendeleo ya mapambano dhidi ya ugaidi, akiwakosoa maadui wa nje na kutoa maelezo kuhusu sheria ya hivi karibuni inayodhibiti desturi za kidini.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Rais wa serikali ya mpito ya Burkina Faso alitoa wito kwa Waislamu kuwa na msimamo wa “wastani” na kushutumu uwepo wa “wachache wa wanaharakati wenye msimamo mkali” nchini. Shambulio la hivi karibuni linalenga jamii ya Waislamu, ambayo imekuwa mstari wa mbele katika uungwaji mkono wa utawala tangu rais huyo alipochukua madaraka mnamo Septemba 2022.
Siku ya Alhamisi, Julai 16, mkuu wa utawala wa kijeshi wa Burkina Faso, Kapteni Ibrahim Traoré, alikuwa Yaagda, kaskazini mwa nchi, ambapo alitoa hotuba ndefu kwa makundi yenye ushawishi katika jamii. Bila kutaja jina lake, alizungumzia kukamatwa kwa Imam Kindo na maandamano yaliyofuata.
Katika hotuba yake, Ibrahim Traoré alibainisha kwamba “kundi dogo la watu wenye msimamo mkali” lilikuwa likisababisha matatizo nchini. “Wana msimamo mkali, lazima mjitenge nao, mapambano yanaanzishwa,” alitangaza. “Hili ndilo lililosababisha ugaidi; tutawasimamisha kuhubiri ikiwa watazungumza ovyo.”
Kulingana na mkuu wa nchi wa Burkina Faso, “ubeberu” unakusudia kutumia dini, haswa Uislamu, “kuiharibu” nchi. Katika miezi ya hivi karibuni, Kapteni Ibrahim Traoré alibainisha mara kwa mara kwamba jeshi hupata nakala za Quran katika vituo vya kigaidi vilivyovunjwa.
Ibrahim Traoré anataka kuwarudisha numbani raia wa Burkina Faso wanaosoma Sharia nje ya nchi
Rais wa mpito ametangaza hatua. Ufadhili wa serikali utatolewa ili kuwasaidia maimamu wanaohubiri “neno jema.” Kuhusu vijana wa Burkinabe wanaosomea elimu ya dini katika nchi za Kiarabu, Kapteni Ibrahim Traoré alitangaza kuwarejesha nyumbani. “Wanafunzi wapatao 800,000 wanasoma Sharia; hawajifunzi kazi. Nitawarudisha, na yeyote ambaye hatarudi atapoteza uraia wa Burkina Faso,” aliongeza.
Tangu mwisho wa mwezi Juni, mwanafunzi yeyote wa Burkinabe anayetaka kusoma nje ya nchi lazima apate idhini kutoka kwa Wizara ya Elimu ya Juu ili kuhakikisha kwamba masomo yao yanakidhi vipaumbele vya serikali.
Uislamu hulengwa mara kwa mara na Serikali
Baada ya mapinduzi ya mwaka 2022, viongozi wa dhehebu la Kisunni katika Uislamu hawakusita kumuunga mkono hadharani Kapteni Traoré. Lakini kwa jamii hii ya Sunni, kutangazwa kwa Siku ya desturi na mila mnamo Mei 15 kulionekana kama dharau ya kweli. Na agizo la kudhibiti sala katika maeneo ya umma ilichangia kuchochea hali hiyo.
“Baada ya kuimarisha mamlaka yake, Kapteni Traoré sasa anawavunja wafuasi wake wa zamani kwa utaratibu,” anabainisha mchambuzi mmoja.
Mchunguzi mwingine anabaini kwamba mapambano haya ya madaraka yanaweza kuendelea. Ibrahim Traoré alionya: baada ya kupigwa marufuku kwa baadhi ya mahubiri na wahubiri wenye msimamo mkali, viongozi wengine wa kidini watalengwa “ikiwa wataendelea.”