Chanzo cha picha, CENTCOM
Saa moja baada ya kutangaza kuanza kwa mashambulizi yake dhidi ya Iran, Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM) ilitangaza kukamilika kwa awamu ya kumi na moja ya mashambulizi hayo.
Siku ya Jumatano asubuhi, wakati mashambulizi hayo yakianza, kulikuwa na ripoti za milipuko kadhaa katika miji kadhaa ya kusini mwa Iran.
Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha usiku wa kumi na moja , Tehran pia ilishuhudia kuwashwa kwa mifumo ya ulinzi wa anga siku ya Jumatano asubuhi, lakini hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa hadi sasa kuhusu shambulio lolote linaloweza kuwa limeilenga mji mkuu huo wa Iran.
Miji mingine ambayo iliripotiwa kushambuliwa ni pamoja na Sirik, Chabahar, Bushehr, Mahshahr, Konarak, Tabriz, Behbahan, na Omidieh.