d

Chanzo cha picha, Reuters/File photo

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema marais wa China na Urusi wamemhakikishia kuwa hawataiuzia Iran silaha.

Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wa Truth Social, Trump alisema Rais wa China, Xi Jinping, alimweleza wakati wa mkutano wao wa hivi karibuni mjini Beijing kuwa China haitatoa wala kuuza silaha kwa Iran kwa hali yoyote.

“Katika mkutano wetu wa hivi karibuni mjini Beijing, Rais Xi aliniambia kwamba hatatoa wala kuuza silaha kwa Iran kwa hali yoyote. Hilo linajumuisha pia kampuni za China,” aliandika Trump.

Trump aliongeza kuwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin, pia alimpa ahadi kama hiyo.

Akizungumzia msaada wa kijeshi kwa Ukraine, Trump alisema: “Watu wanafikiri siuzi silaha kwa Ukraine. Ninaziuza kwa nchi za NATO. Wanalipa bei kamili kwa silaha hizo na sijui wanazifanyia nini baadaye.”

Trump pia alisema haamini kuwa China na Urusi zinahusika moja kwa moja katika vita dhidi ya Iran.

“Mataifa hayo mawili makubwa ambayo mara nyingi hutajwa kuhusishwa na Iran, sidhani kama yanahusika. Kama yangekuwa yanahusika, hakika isingekuwa kwa maslahi yao wenyewe,” alisema.

Hata hivyo, China na Urusi hazijatoa tamko rasmi kuthibitisha kauli za Trump kuhusu madai hayo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *