Simanzi imetawala nchini Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla, kufuatoa kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo, Raila Amolo Odinga.

Odinga, mwenye umri wa miaka 80, amefariki dunia nchini India, alipokuwa akipatiwa matibabu.

Raila, maarufu kama ‘RAO’, atakumbukwa kwa ushawishi wake aliokuwa nao kwenye ulingo wa siasa ndani na nje ya Kenya.

Mwanasiasa huyo, aliyezaliwa Januari 7, 1945, amekuwa nguzo muhimu katika historia ya siasa ya nchi hiyo.

Raila, ambaye pia alifahamika kwa jina la ‘Tinga’, amekuwa nguzo muhimu katika siasa za nchini Kenya kutokana na harakati zake za siasa ambazo zimedumu kwa zaidi ya miaka 40.

Kwa kiasi fulani, unaweza kusema kuwa amerithi harakati hizo kutoka kwa baba yake mzazi, Hayati Jaramogi Oginga Odinga, ambaye alikuwa mmoja wa wapigania uhuru wa Kenya na baadaye kuja kuwa Makamu wa Kwanza wa taifa hilo.

Ni harakati hizo hizo, ambazo zilimfanya afungwe jela kwa nyakati tofauti.

Raila, ambaye alipenda kujifananisha na Cesc Fabreags, kiungo mchezeshaji wa zamani wa klabu ya Arsenal, akisisitiza kuwa yeye ni kiungo muhimu katika kutengeneza safu ya uongozi mahiri nchini Kenya.

Mwanasiasa huyo aliwahi kugombea nafasi ya Urais vipindi vitano tofauti, bila mafanikio yoyote.

Licha ya hali hiyo, RAO amekuwa na nafasi na mchango wa pekee kwenye siasa za Kenya.

Kabla ya uchaguzi wa mwaka 2002, chama cha Raila kilijiunga na serikali ya rais wa awamu ya pili Daniel Arap Moi, huku yeye akipewa nafasi ya Uwaziri wa Nishati.

Mwaka 2002 akasaidia upinzani ulioongozwa na rais wa awamu ya tatu Mwai Kibaki kupata ushindi mkubwa dhidi ya Uhuru Kenyatta na chama cha KANU.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *