Waziri wa Sheria Edasso Rodrigue Bayala amesema mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kushiriki katika  vitendo vya ushoga  au vitendo vinavyofanana atakabiliwa na  adhabu ya kifungo cha miaka 2 hadi 5 pamoja na faini, huku wageni watakaobainika na kosa hilo wakifukuzwa nchini humo.

Ushoga tayari umepigwa marufuku katika zaidi ya nchi 30 kati ya 54 za Afrika. Mashirika ya haki za binadamu yamekosoa vikali hatua hizi, yakitahadharisha kwamba zinakiuka misingi ya haki na usawa na zinachochea unyanyapaa na ukatili dhidi ya watu wa jamii ya LGBTQ+.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *