Ndege ya safari za ndani ya kwanza ya kibiashara ya kampuni ya Badr Airlines ilipangwa kufanyika Oktoba 22, lakini mashambulizi ya ndege zisizo na rubani mapema Jumanne na Jumatano yaliashiria kuendelea kwa udhaifu wa uwanja huo.
RSF imeshambulia miundombinu ya kijeshi na ya kiraia katika maeneo yote yanayodhibitiwa na jeshi kwa kutumia ndege zisizo na rubani wakati ikipigania kuimarisha udhibiti wa eneo la Darfur.
Chanzo cha shirika la ndege kilisema safari hiyo ilicheleweshwa kwa siku kadhaa kwa sasa, huku hali ikiendelea kufuatiliwa.
Mapema wiki hii, kampuni hiyo ilisema kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook kwamba ilikuwa imefanya majaribio ya ndege katika uwanja huo. Na kwamba ndege za safari za ndani pekee ndizo zimepangwa kwa wakati huu.
Mkuu wa jeshi na kiongozi wa Sudan Jenerali Abdel Fattah al-Burhan alizuru uwanja wa ndege siku ya Jumanne baada ya mashambulizi hayo, hata hivyo taarifa ya jeshi ilisema mashambulizi hayo yaliweza kuzuiwa.
Vyanzo vya usalama vilisema uharibifu kutoka kwa mashambulizi ya siku zote mbili ulikuwa mdogo.