Viongozi hao waliongoza kwa pamoja Mkutano wa 11 wa Kamati ya Juu wa Kimkakati Uturuki – Qatar, ambapo walitia saini mikataba mipya ya ushirikiano, ikijumuisha: Makubaliano ya Mpango wa Maendeleo ya Kimkakati, Makubaliano ya Ushirikiano wa Sekta ya Ulinzi, Azimio la Pamoja la Mkutano wa Kamati Kuu ya Kimkakati, na Taarifa ya Pamoja ya Mawaziri kati ya wizara za biashara za nchi hizo mbili.

Rais wa Uturuki pia alihudhuria chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima yake na amiri wa Qatar.

Inayohusiana

Oman

Sehemu ya mwisho ya ziara ya Erdogan katika Ghuba ilikuwa jijini Muscat, Oman, ambako alipokelewa kwa heshima kamili na Sultani Haitham bin Tariq katika Kasri la Al Alam.

Viongozi hao wawili walijadili masuala ya pande mbili na ya kikanda, wakisisitiza mtazamo wao wa pamoja kuhusu suala la Palestina na umuhimu wa diplomasia inayojikita kwenye mazungumzo.

Erdogan alisifu nafasi ya Oman kama mpatanishi katika migogoro ya kikanda na kusema kuwa Uturuki na Oman zitaendelea kuunga mkono juhudi za kufanikisha suluhisho la mataifa mawili huko Gaza.

Erdogan alimkabidhi Sultani Haitham gari jekundu la umeme aina ya Togg kabla ya kushuhudia hafla ya kusaini makubaliano yanayogusa maeneo mbalimbali kama ulinzi, nishati, madini, viwanda, elimu ya juu, vyombo vya habari na masuala ya viza.

Miongoni mwa mikataba yaliyosainiwa ni:

Mkataba kuhusu Madini Muhimu, Mkataba wa Ushirikiano wa Kijeshi, Mkataba wa Ushirikiano wa Viwanda, Mkataba wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, Mktaba wa Ulinzi wa Ushindani katika Soko, Mkataba kuhusu Vyombo vya Habari na Mawasiliano, Mkataba wa Ushirikiano katika Sekta ya Ulinzi, Mkataba wa Ushirikiano wa Kistratejia kati ya Mfuko wa Uturuki na Mamlaka ya Uwekezaji ya Oman, pamoja na mikataba kadhaa ya umiliki wa hisa na ushirikiano kati ya kampuni za Uturuki na Oman, ikiwemo OYAK, Amber Limited, Uzbek-Oman Investment Company na Oman Food Investment Holding, Mkataba na Kampuni ya i ya Innovance Information Technologies Inc. na Kampuni ya Mawasiliano ya Oman, na Mkataba wa Ushirikiano wa Upatikanaji wa Sehemeu Ardhi kwa ajili ya Taasisi ya Maarif ya Uturuki kuanzisha shule nchini Oman.

Azimio ya pamoja pia yalisainiwa: moja kuhusu kuanzishwa kwa Baraza la Uratibu na jingine kuhusu msamaha wa viza kwa wamiliki wa pasipoti za kawaida.

Baada ya kushiriki chakula cha mchana kilichoandaliwa na Sultani Haitham, Erdogan aliondoka Muscat na kurejea Uturuki, na hivyo kukamilisha ziara yake ya siku tatu ya Ghuba.

Inayohusiana

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *