
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, siku ya Jumanne, Novemba 4, amempongeza mwenzake wa Côte d’Ivoire, Alassane Ouattara, kwa kuchaguliwa tena, na kutoa wito wa kuendelea kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Rais wa Jamhuri amempigia simu Rais wa Jumanne, Novemba 4, Alassane Ouattara, kumpongeza kwa kuchaguliwa tena kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25 na Baraza la Katiba,” Ikulu ya Élysée imesema.
“Ametangaza nia yake ya kuendelea kufanya kazi naye ili kuimarisha na kufufua ushirikiano wa karibu kati ya nchi hizo mbili, pamoja na kukuza mazungumzo kuhusu masuala ya kimataifa,” ofisi ya raiswa Ufaransa imeongeza.
Alassane Ouattara ambaye alichaguliwa tena Jumatatu, Novemba 27, kama rais wa Côte d’Ivoire kwa karibu asilimia 90 ya kura, kufuatia uchaguzi ambao wapinzani wakuu hawakushiriki. Kwa kuwa wagombea wawili wakuu wa upinzani hawakuwepo, idadi ya wapiga kura ilikuwa zaidi ya asilimia 50, kiwango kinacholingana na kile cha chaguzi zilizopita.