Uhamishaji huo ni sehemu ya mpango wa Rais Daniel Noboa kuyadhoofisha magenge ya kihalifu amabyo yamekuwa yakiendesha shughuli zao ndani ya magereza ya nchi hiyo ya Amerika Kusini kwa muda mrefu.

Mamia ya wafungwa wamepoteza maisha kutokana na magenge hayo katika miaka ya hivi karibuni.

Rais Noboa alichapisha  picha ya Glas akiwa kwenye gereza hilo jipya katika mtandao wa X, hatua iliyolalamikiwa na wakili wa makamu huyo wa zamani wa rais kama kitendo cha uvunjaji haki za binaadamu.

Mnamo mwezi Juni, mahakama ilimuhukumu Glas kifungo chengine cha miaka 13 kwa ubadhirifu wa fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa maeneo yaliyoathirika kwa tetemeko la ardhi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *