Kiongozi wa harakati za kujitenga ahukumiwa kifungo maisha kwa mashtaka ya ugaidi nchini Nigeria
Mahakama ya Nigeria Alhamisi imemhukumu Nnamdi Kanu, kiongozi wa harakati za kujitenga za Indigenous People of Biafra (IPOB), yaani Watu wa Asili wa Biafra, kifungo cha maisha jela baada ya kumhukumu kwa mashtaka yote saba yanayohusiana na ugaidi.