Ofisi ya Rais wa Afrika Kusini ilitania na kusema kuwa nchi hiyo “itachukua likizo” kutoka kwa G20 wakati Rais Donald Trump anapoongoza jukwaa hilo, baada ya utawala wa Trump kuthibitisha kwamba haitaialika Afrika Kusini kushiriki.
Marekani imechukua hatamu ya uongozi unaozunguka wa 20 wiki iliyopita, baada ya kugoma kuhudhuria kilele cha mkutano huo ulioandaliwa na Rais Cyril Ramaphosa Johannesburg.
“Wakati huu mwaka ujao, Uingereza itachukua uenyekiti wa G20. Tutaweza kujihusisha kikamilifu na mambo yanayowahusu ulimwengu mzima,” alisema msemaji wa Ramaphosa, Vincent Magwenya.
“Kwa sasa, tutapumzika hadi tutakaporudi kwenye mpango wa kawaida,” aliandika kwenye mitandao ya kijamii.
Mahusiano kati ya Washington na Pretoria yamekuwa mabaya mwaka huu baada ya Trump kurudia madai ya uongo kuhusu “mauaji ya wazungu” nchini Afrika Kusini na kukosoa nchi hiyo kwa sera zake za kukabiliana na ukosefu wa usawa wa rangi.