Lumbala alipatikana na hatia katika mahakama ya jinai ya Paris kwa tuhuma za uhalifu dhidi ya ubinadamu.

Wakili wa Lumbala, ambaye ana siku kumi za kukata rufaa, ameitaja hukumu hiyo kuwa kali.

Lumbala mwenye umri wa miaka 67 aliongoza kundi la waasi wa Kongo kwa ajili ya Demokrasia ya Kitaifa, lililodaiwa kuungwa mkono na Uganda na kushtumiwa kwa ukatili dhidi ya raia, hasa kwa kuzilenga jamii za makabila madogo ya Nande na Bambuti mashariki mwa Kongo kati ya mwaka 2002 na 2003.

Waathiriwa wa dhulma hizo wamepongeza hukumu hiyo na kusema hatimaye haki imepatikana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *