Nchini Madagascar, wagonjwa watano wa Mpox, pia unaojulikana kama virusi vya homa ya nyani, wamethibitishwa na Wizara ya Afya ya Umma. Wagonjwa kumi na mmoja wanaoshukiwa kuambukizwa virusi hivyo pia wamerekodiwa. Wagonjwa wote walipatikana na virusi katika jiji la Majunga, mapumziko ya ufukweni kaskazini magharibi mwa nchi.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Antananarivo, Guilhem Fabry

Nchini Madagascar, visa vya kwanza vimethibitishwa katika kitongoji kilicho kwenye ufuo wa bahari wa Majunga, kufuatia vipimo vilivyofanywa na Taasisi ya Pasteur na Maabara ya Uchambuzi wa Kimatibabu ya Madagascar. Watu wanne wamelazwa hospitalini, lakini hali yao “imeimarika kwa kiasi kikubwa,” kulingana na mamlaka ya afya.

Virusi hivi huambukizwa kupitia mgusano wa karibu na mtu aliyeambukizwa: kupitia mate, kupiga chafya, au wakati wa kujamiiana. Mamlaka ya afya sasa wanataka kuzuia kuenea ugonjwa huo kote nchini.

Wagonjwa wengine wamewekwa kando ili kuzuia maambukizi ya virusi hivi, ambayo husababisha, miongoni mwa mambo mengine, homa kali na vipele vya ngozi.

Lengo la serikali sasa ni kudhibiti mlipuko huko Majunga, kwani msimu wa likizo unahimiza mikusanyiko na unaambatana na usafiri mkubwa kati ya mikoa. Hali hii inasababisha wasiwasi mkubwa miongoni mwa wadau wa utalii. Fabhie Vonjy Soloniaina, meneja wa hoteli jijini, anakiri kwamba hapo awali “aliingiwa na hofu.”

“Tuliposikia kuhusu visa vya kwanza vya Mpox, tuliingiwa na hofu. Tuliona picha za watu kwenye mitandao ya kijamii, wakiwa na madoa mwilini kote.” “Lakini kisha tulichukua tahadhari: tunatumia kitakasa mikono kwenye mlango wa hoteli na pia tunasambaza kondomu kwa wanandoa,” anaelezea mdau huu wa utalii.

“Ninaisihi mamlaka husika kusambaza barakoa kwa kila mtu kwa sababu virusi hivi vinaambukia sana na vitaenea ikiwa hatutachukua hatua sasa, na itatusababishia tatizo kubwa, haswa kwa utalii na biashara yetu. Ninaogopa itakuwa kama UVIKO, na itaharibu kila kitu. Natumai ugonjwa lutapungua na kwamba watapata suluhisho haraka iwezekanavyo.”

Siku ya Jumatano, Dkt. Désiré Rakotoarimino, Mkurugenzi Mkuu wa Tiba ya Kinga, aliwataka watu kuheshimu hatua za kinga, ikiwa ni pamoja na kuvaa barakoa na kunawa mikono mara kwa mara. Uchunguzi wa afya pia umetangazwa katika bandari na uwanja wa ndege wa Majunga.

Hizi ni kesi za kwanza za Mpox kuripotiwa nchini Madagascar tangu kuibuka tena kwa mlipuko huo Afrika ya Kati mnamo mwezi Agosti 2024.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *