[ad_1]

Makamu wa Rais wa Tume ya Ulaya Kaja Kallas alisema kuwa "kuna dalili" kwamba ukiukaji wa Urusi wa anga ya Poland "ilikuwa ya kukusudia, sio bahati mbaya."

Chanzo cha picha, Reuters

Vikosi vya Poland na NATO vilidungua ndege zisizo na rubani katika anga ya Poland siku ya Jumatano wakati wa shambulizi la anga la Urusi dhidi ya Ukraine, nchi ambayo inapakana nayo.

Mamlaka ya Poland ilielezea uvamizi huo kama “ukiukaji usio na kifani” wa eneo lao na ulianzisha Kifungu cha 4 cha NATO, ambacho kinaruhusu mashauriano rasmi na muungano wakati uadilifu wa eneo la nchi wanachama unatishiwa.

Rais wa Poland Donald Tusk alionya kwamba hali ni “ya hatari zaidi kuliko hali yoyote iliyopita” na akabainisha kuwa matarajio ya mzozo mkubwa wa kijeshi “yamekaribia kuliko wakati wowote tangu ”Vita vya pili vya Dunia .”

Pavel Muravyeika, naibu waziri wa ulinzi wa Belarus, mshirika wa Urusi, alisema ndege zisizo na rubani ziliingia katika anga ya Poland kwa bahati mbaya baada ya mifumo yao ya urambazaji kuzuiwa.

[ad_2]

Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *