
Muungano Huru wa Madaktari (Sylimed) nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), umeitisha mgomo usio na kikomo katika sekta ya umma, kuanzia Juni 11. Muungano huo unapinga kushindwa kwa serikali kujibu madai yake kuhusu mishahara, mazingira ya kazi, na rasilimali zilizotengwa kwa sekta ya afya. Mgomo huu unakuja wakati eneo la mashariki mwa DRC linaendelea kukumbwa na mlipuko wa Ebola.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Karibu madaktari 2,500 wa sekta ya umma hawajapokea mishahara yao kwa miezi kadhaa, kulingana na chama cha wafanyakazi kinachoitisha mgomo. Wanalaani mishahara na marupurupu yasiyolipwa, mazingira duni ya kazi, na hatari ya taaluma hiyo, huku madaktari wakiwa mstari wa mbele kupambana na mlipuko hatari wa Ebola nchini DRC, anasema Dkt. André Kasongo Kasomboyi, Katibu Mkuu wa Sylimed, akizungumza na Alexandra Brangeon: “Hawalipwi. Bima ya afya bado haijalipwa katika mikoa karibu yote. Imekuwa zaidi ya miezi 11, na tunapaswa kupambana na virusi. Hatutaendelea kuwahamasisha raia kwenda kupambana na Ebola wakati hawajalipwa.”
Huduma za dharura zitaendelea kufanya kazi
Madaktari watatu wamefariki Ituri tangu kuanza kwa mlipuko huo mwezi mmoja uliopita. Dkt. aliyefariki hivi karibuni, ni Dkt. Jackson Ngoy Ngoy, ambaye alifariki siku ya Jumapili iliyopita huko Nyakunde, karibu na Bunia. Kwa daktari katika mji mkuu wa mkoa wa Ituri – ambaye anataka kubaki bila jina – mazingira haya mabaya ya kazi yanaathiri ari ya wafanyakazi wa afya: “Tunakaa miezi kadhaa bila malipo, ingawa hali tunazofanyia kazi ni mbaya. Mimi, ninayezungumza nawe kutoka hapa, sina hata mshahara. Ninapokea tu pesa ya ziada kazini, na pesa hizo zinaweza kupunguzwa wakati wowote. Hakuna motisha, ingawa tunahatarisha maisha yetu.”
Hata hivyo, chama hicho kinahakikisha kwamba huduma za dharura zitaendelea kufanya kazi ili kuhakikisha kwamba visa vikubwa zaidi vinashughulikiwa.
Shirika la Afya Duniani (WHO), limeanzisha tahadhari ya afya ya kimataifa ili kukabiliana namlipuko huo ambao umekuwa ukiendelea tangu katikati ya mwezi Mei nchini DRC na katika baadhi ya nchi jirani kama vile Uganda, huku, kulingana na WHO, zaidi ya wagonjwa 500 walithibitishwa kuambukizwa virusi vya ugonjwa wa Ebola, ikiwa ni pamoja na vifo kadhaa.