Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan amesema kuwa amemwambia Rais wa Marekani Donald Trump katika mazungumzo kwa njia ya simu kwamba Venezuela haitakiwi kuingizwa katika hali ya kutokuwa na usalama baada ya kumpindua kiongozi wake Nicolas Maduro.

Akizungumza baada ya mkutano wa baraza la mawaziri siku ya Jumatatu, Erdogan alionya kuwa kukiuka uhuru wa nchi na kudharau sheria za kimataifa ni hatari sana na huenda kukasababisha “matatizo makubwa duniani.”

“Uturuki haiungi mkono hatua zozote za ukiukwaji wa sheria ya kimataifa,” Erdogan alisema, akiongeza kuwa Uturuki inajitahidi kufanya kile kilicho bora kwa Uturuki na “taifa la ndugu zetu wa Venezuela.”

Amesema Uturuki inaunga mkono “watu wa Venezuela marafiki katika kupambania mafanikio, amani na ustawi,” akieleza kuwa Maduro na watu wa Venezuela waliwahi kuonesha urafiki kwa Uturuki hapo awali.

Erdogan pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia sheria za utawala za kimataifa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *